Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Semistocles Kaijage amebadilisha majimbo ya majina matatu.
Jaji Kaijage ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habarri kuhusiana na ratiba ya kuchukua fomu kwa ngazi ya urais, ubunge na udiwani.
Jimboa Chilonwa ambalo kwa sasa litaitwa Chamwino, jimbo la Mtera litaitwa Mvumi na jimbo la kijitopele lililopo wilaya ya Magharibi B litaitwa Pangawe.
Aidha, Jaji Kaijage ametangaza ratiba ya kuchukua na kurejesha fomu kwa nafasi ya urais, ubunge na udiwani.
Amesema kwa nafasi ya urais fomu zitaanza kutolewa kuanzia Agosti 5 hadi 25, 2020 jijini Dar es Salaam na fomu za ubunge na udiwani zitatolewa kuanzia Agosti 12 hadi 25, 2020.
#HABARI Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imebadilisha majina ya majimbo matatu, likiwemo jimbo la Chilonwa, ambalo kwa sasa linaitwa Chamwino, Jimbo la Mtera limebadilishwa na kuitwa Mvumi, na Jimbo la kijitopele lililopo Wilaya ya Magharibi B linaitwa jimbo la Pangawe. pic.twitter.com/T3C9lhuWVq
— EastAfricaTV (@eastafricatv) July 23, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/23/mwenyekiti-wa-tume-ya-uchaguzi-jaji-kaijage-amebadilisha-majina-majimbo-matatu/
No comments:
Post a Comment