Benjamin Mkapa alifariki alipokuwa akipata matibabu katika hospitali moja jijini Dodoma, Ijumaa, Julai 24. Picha: Hisani
Kifo chake kilitangazwa na Rais wa Jamhuhuri ya Tanzania Johhn Pombe Magufuli akitangaza siku saba za kumuomboleza
Moussa Faki, aliyekuwa mwenyekiti wa AUC, Rais Uhuru Kenyatta, Raila Odinga, Yoweri Museveni ni kati ya viongozi waliomuomboleza
Viongozi kote Afrika wameungana na jamuhuri ya Tanzania katika kumuomboleza aliyekuwa rais wa nchi hiyo Benjamin Mkapa aliyefariki Ijumaa, Julai 24 hospitalini alikokuwa akipata matibabu.
Habari kuhusu kifo chake kilitangazwa na Rais John Pombe Magufuli katika idhaa ya taifa ya TBC huku akitangaza kuhusu siku saba ya maombolezi.
Nimesikitishwa na kifo cha Mzee wetu Benjamin Mkapa (Rais Mstaafu wa Awamu ya 3). Nitamkumbuka kwa mapenzi yake makubwa kwa Taifa, ucha Mungu, uchapakazi na utendaji wake katika kujenga uchumi. Hakika Taifa limepoteza nguzo imara. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.
— Dr John Magufuli (@MagufuliJP) July 23, 2020
Viongozi wa Afrika wamejitokeza kwa kila njia kumuomboleza kiongozi huyo kwa kutuma jumba za rambi rambi kwa ndugu jamaa na marafiki.
Just in: Former President of Tanzania Benjamin Mkapa has passed away. pic.twitter.com/Y1ivDNogqL
— Samira Sawlani (@samirasawlani) July 23, 2020
Aliyekuwa mwenyekiti wa muungano wa AUC, Moussa Faki Mahamat alimtaja hayati Benjamin Mkapa kama mweka Amani mkuu katika eneo la Afrika Mashariki.
‘’Ni kwa huzuni kubwa, nimepata kujua kuhusu kifo cha Mzee Benjamin Mkapa, aliyekuwa Rais wa Tanzania,’’ Mousa aliandika.
Mzalendo anayekumbukwa haswa kwa kuwa mweka Amani Afrika Mashariki. Maombi yangu yaendee familia, Watanzania pamoja na serikali ya Tanzania,’’ aliongezea.
Rais Uhuru Kenyatta alimtaka hayati Mkapa kama mdumishi wa Amani na aliyefanya kila nia kupigisha Afrika mashariki hatua nyingi.
Aliyekuwa Waziri mkuu wa Kenya, Raila Odinga alimkumbuka Mkapa kama rafiki mkuu wa Kenya na mzalendo wa ajabu.
When Kenya was on the brink of the precipice after a bungled presidential election of 2007, you came through for us. Together with other eminent persons of our continent, you worked tirelessly to save Kenya from going. We are saddened by your death Mzee Benjamin Mkapa #RIPMkapa. pic.twitter.com/BpAJP4UyP8
— The ODM Party (@TheODMparty) July 24, 2020
Kifefe Kizza Besigye naye hakuachwa nyuma, Mtetezi mkuu wa haki za kibinadamu Uganda alimtaja Mkapa kama kiongozi aliyeacha kumbukumbu wa huduma na uadilifu mkubwa.
Viongozi wengine walioungna na Jamuhuri ya Tanzania katika kumuomboleza kiongozi wao ni pamoja na wabunge, maseneta na viongozi mbali mbali mbali.
Derision, cynicism, prejudice, stereotyping and hunger for stories of failure than of success will be the undoing of democratic progress on the continent ~ Benjamin Mkapa
We have lost a pan africanist! #RIPMzeeMkapa— Raila Odinga Junior (@Railajunior) July 24, 2020
Benjamin Mkapa was a good, selfless & decent man … A rare virtue for a politician … To him, leadership was public service & when his term ended, he retreated quietly to the sunset except when he came to stop Kenya from descenting to hell in 2007 .. #RIPMzeeMkapa
— Donald B Kipkorir (@DonaldBKipkorir) July 24, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/24/benjamin-mkapa-viongozi-wa-afrika-waungana-na-watanzania-kumuomboleza-aliyekuwa-rais-wao/
No comments:
Post a Comment