Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe amesema yeye na familia yake imeshtushwa na kusikitishwa sana na kifo cha ghafla cha Rais Mstaafu Benjamin Mkapa.
“Tutamkumbuka kwa akili kubwa ya uchambuzi, uwezo wake wa kusuluhisha migogoro barani Afrika na uwanadiplomasia uliotukuka. Poleni wanafamilia RIP,” aliandika Membe katika ukurasa wake wa Twitter.
Rais Mstaafu Mkapa amefariki usiku wa kuamkia leo akiwa amelazwa hospitali kwa ajili ya matibabu jijini Dar es Salaam.
Mimi na Familia yangu tumestushwa na kusikitishwa sana na kifo cha ghafla cha Mzee wetu Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa. Tutamkumbuka kwa akili kubwa ya uchambuzi, Uwezo wake wa kusuluhisha migogoro barani Afrika, na Uwanadiplomasia uliotukuka. Poleni wanafamilia.RIP- BMW.
— Bernard K. Membe (@BenMembe) July 24, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/24/membe-tutamkumbuka-rais-mstaafu-mkapa-kwa-akili-kubwa-ya-uchambuzi/
No comments:
Post a Comment