Friday, July 24, 2020

Waandamana Kupinga Mshindi Kura Za Maoni Ubunge

Mbunge wa Jimbo la Magomeni akabidhi Basi Jimboni - ZanziNewsIkiwa zimepitia siku kadhaa baada ya kunalizia kwa uchaguzi wa ngazi ya jimbo wa kupendekeza majina ya wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) watakaogombea ubunge na uwakilishi kwenye uchaguzi ujao mapema mwezi Oktoba.

Wakazi wa jimbo ka Magomeni visiwani Zanzibar wameandamana mpaka nyumbani kwa mshindi wa uchaguzi huo Jamal Kassim kwa lengo la kupinga ushindi wake baada ya uchaguzi  uliofanywa na wa wajumbe chama.

Waandamaji walioandama na ngoma na mabango wamesema hawezi kukubari Jamali kupewa nafasi ya kuongoza tena kwenye jimbo hilo aliloliongoza kwa miaka kadhaa.

Bado mchakato wa ndani ya chama wa kutafuta wagombea unaendelea mpaka pale majina kutoka hamashauri kuu ya chama hicho yatakapoletwa kwenye ngazi za awali za chama kwa ajili ya kutagaza kwama wagombea rasmi wa chama hicho.

CHANZO: JamiiForums



source http://www.bongoleo.com/2020/07/25/waandamana-kupinga-mshindi-kura-za-maoni-ubunge/

No comments:

Post a Comment