Tuesday, July 28, 2020

Rais Magufuli Afunguka Kauli Ya Mwisho Aliyoambiwa Na Mzee Mkapa

Photo by Clouds FM🇹🇿 on July 28, 2020. Image may contain: 3 people, text that says '7 cloudstv'


Rais wa John Magufuli amesema aliongea na Rais wa awamu ya tatu hayati Benjamin Mkapa siku chache akiwa hospitalini kabla ya kifo chake Usiku wa kuamkia Julai 24,2020.

Rais Magufuli amesema alipoongea na hayati Mkapa alimtoa wasiwasi na kumuambia asijali na yupo salama.

“Mzee Mkapa niliongea nae akiwa Hospitalini kwa simu akaniambia ‘John usiwe na wasiwasi naendelea vizuri’ sikujua kuwa maneno yake yalikuwa ni ya kuniaga, namshukuru Mungu kazi ameikamilisha.. Mkapa, Mwinyi,Kikwete mara nyingi tunakuwa nao pamoja leo Mkapa hayupo”

Mwili wa Rais Mstaafu  Benjamin Mkapa unatarajiwa kusafirishwa leo kwenda kijijini kwao Lupaso mkoani Mtwara kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika Julai 29,2020.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/28/rais-magufuli-afunguka-kauli-ya-mwisho-aliyombiwa-na-mzee-mkapa/

No comments:

Post a Comment