Wednesday, July 22, 2020

Msigwa awapongeza wanachama wa CCM kwa kuwapiga chini waliohamia

 

Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Iringa mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa, amewapongeza wanachama wa kawaida wa Chama cha Mapinduzi kwa kutowachagua waliohamia kwenye chama chao.

“Kwa mara ya kwanza nichukue fursa hii kuwapongeza sana wanachama wa kawaida wa CCM katika maeneo mbalimbali kwa kuwapa walichostahili hawa wahamiaji,” aliandika Msigwa katika ukurasa wake wa Twitter.

Msigwa amesema watu hao hawana msimamo,  fadhila wala nidhamu.

“Mmeonyesha jinsi ambavyo mmewapuuza, hongera kwa hilo,”aliandika Msigwa.

 



source http://www.bongoleo.com/2020/07/22/mchungaji-msigwa-awapongeza-wanachama-wa-ccm-kwa-kuwapiga-chini-waliohamia/

No comments:

Post a Comment