Tuesday, July 21, 2020

Jamaa Avamia Afisi ya Bosi kwa Panga Kudai Mshahara wa Miezi Mitano( Video)

Angry man storms boss's office with machete, demands 5-months salary in viral video

Jamaa huyu ambaye hakutambulika aliivamia afisi ya bosi akiwa na panga mkononi

Alidai kuwa bosi wake alikuwa hajamlipa kwa miezi sita

Janga la corona limekuwa tatizo kuu, umaskini ukidhihirika wazi na hivyo hasira za kila namna kujaa nyosoni.

Kando na wengi kukosa nafasi za ajira, wengine wamesalia miezi kadhaa bila malipo waajiri wakishindwa la kufanya.

Jamaa mmoja amezua gumzo katika mitandao ya kijamii baada ya kufika katika afisi ya bosi wake akiwa mejihami kwa panga akitaka alipwe mshahara wake wa miezi mitano mara moja.

Katika video hiyo iliyosambaa kwenye mtandao wa twitter na Facebook Jumanne, Julai 21, jamaa huyo anaonekana akiingia kwenye afisi hiyo kabla kuanza kujibizana na bosi mwenye lahaja ya kihindi.

“Umekuja na panga? Weka panga kando kwanza,

“Niweke panga chini kwa nini? Nakuambia kabla polisi aingie hapa nitakuwa nimekuua,’’ anasema kwenye video hiyo.

Baada ya kugndua kuwa bwana huyo ameshika mori tayari kumvamia, bosi huyo anasikika akiwaomba wafanyikazi wengine kumpa msaada.

“Mimi nataka mshahara yangu ya mwezi wa tatu, wa nne, wa tano, wa sita na wa saba,’’ bwana huyo anongezea kwa hasira.

Wanamitandao walitofautiana kuhusiana na hatua aliyoichukua bwana huyo, baadhi wakimuunga mkono huku wengine wakimshambulia vikali kwa kukiuka sheria.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/21/jamaa-avamia-afisi-ya-bosi-kwa-panga-kudai-mshahara-wa-miezi-mitano-video/

No comments:

Post a Comment