Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ametoa muda wa wiki moja kwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Ndalichako, kuhakikisha anakutana na wakuu wa vyuo vikuu nchini.
Majaliwa amesema akutana na vyo hivyo ili kubaini vyuo ambavyo vimeshindwa kuwasilisha mchango wa wanafunzi kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Imeelezwa kuwa wanafunzi wa vyuo wamelipa michango yao lakini mpaka sasa vyuo havijawasilisha NHIF.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa muda wa wiki moja kwa Wizara ya Elimu kukutana na Wakuu wa Vyuo Vikuu nchini ili kubaini vyuo ambavyo vimeshindwa kuwasilisha michango ya wanafunzi katika Mfuko wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) licha ya wanafunzi kulipa fedha hizo. pic.twitter.com/COmMtViyq1
— Radio One Stereo (@RadioOneStereo) August 9, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/08/09/waziri-mkuu-majaliwa-ampa-siku-saba-waziri-ndalichako/
No comments:
Post a Comment