Thursday, August 13, 2020

Mlinzi wa ofisi ya Chadema iliyoteketea kwa moto hajulikani alipo

Mlinzi wa ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini hajajulikana alipo baada ya ofisi kulipuliwa kwa petroli na kuteketea kwa moto.

Aliyekuwa Meya wa Ubungo, Bonifance Jacob amesema wanamuombea mlinzi wao aweze kupatikani akiwa mzima.

Jacob aliandika ujumbe huo katika ukurasa wake wa twitter huku akitoa pole kwa uongozi wa Chadema Arusha na Mwenyekiti wa Kanda Kaskazini, Godbless Lema kwa kuchomewa ofisi yao.

Usiku wa kuamkia leo ofisi hiyo imedaiwa kulipuliwa na petroli na watu wasiojulikana na kuteketea.

Chadema imesema inaendelea  na uchunguzi kubaini hatari zaidi inayoweza kuwa imewekwa.



source http://www.bongoleo.com/2020/08/14/mlinzi-wa-ofisi-ya-chadema-iliyoteketea-kwa-moto-hajulikani-alipo/

No comments:

Post a Comment