Tuesday, August 11, 2020

Serikali Nzima ya Lebanon Yajiuzuli Kufuatia Mlipuku wa Beirut, Habari Kamili

Lebanese president asks Hassan Diab to form government | News | Al ...

Waziri Mkuu Hassan Diab aliongoza katika kujiuzulu Jumatatu, Agosti 10

Rais Michel Aoun alimuomba Diab kushikilia wadhifa huo kabla kufanyika uteuzi mwingine

Diab amechukua hatua ya kujiuzulu kufuatia maandano makali ya wananchi baada ya mlipuko wa Beirut

Waziri Mkuu wa Lebanon Hassan Diab alichukua nafasi ya kipekee Jumatatu, Agosti 10 kutangaza kuhusu kujiuzulu kwa serikali yake nzima.

Diab alichukua hatua hiyo wiki moja tu baada ya mlipuko wa ajabu katika mji mkuu wa Beirut uluowaua zaidi ya watu 150, kuwajeruhi maelfu na kuwaacha wengi bila makazi.

Michel Aoun elected president of Lebanon, ending 29-month vacuum ...

Rais Michel Auon alimuomba Diab kushikilia nafasi  hiyo kama kaimu hadi wakati serikali nyingine inapoteuliwa kuchukua hatamu. Picha: Hisani

Diab aliamua kujiuzulu pamoja na serikali yake nzima huku maandamano yakishika kasi nchini humo, wananchi wakikabiliana na maafisa wa polisi katika mvutano mkali.

Licha ya kukubali hatua hiyo ya kujiuzulu, Rais Michel Auon wa nchi hiyo alimuomba Diab kushikilia nafasi  hiyo kama kaimu hadi wakati serikali nyingine inapoteuliwa kuchukua hatamu.

Kujiuzulu kwa serikali hiyo kunajiri wakati mataifa mbali mbali yakiongozwa na Rais wa Jamuhuri ya Ufaransa Emmanuel Macron akiandaa mkutano wa kimtandao na kuahidi TSh 600 bilioni kuisaidia nchi hiyo.

Kupitia kwa waziri wa mambo ya nje, Jean-Yves Le Drian, Rais huyo  aliiomba serikali ya Lebanon kuhakikisha kuwa msaada huo unakwenda moja kwa moja kwa wananchi.

Rais wa Amerika Donald Trump pia aliahidi kutuma msaada wake kwa serikali hiyo.

Je, waunga mkono hatua ya kujiuzulu kwa serikali ya Lebanon?



source http://www.bongoleo.com/2020/08/11/serikali-ya-lebanon-yajiuzuli-kufuatia-mlipuku-wa-beirut-habari-kamili/

No comments:

Post a Comment