Tetemeko ardhi limeripotiwa kutokea jijini Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Arusha muda mfupi uliopita na kuibua sitofahamu kwa wananchi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotufikia hadi sasa hakuna madhara yoyote yaliyoripotiwa.
Mjiolojia Gabriel Mbogoni amesema mpaka sasa bado hawajasoma kwenye mfumo kujua ni la kiwango gani.
Tetemiko hilo zimezua hekaheka kwa wananchi huku ikiekezwa kwa kuwa wahindi wanaoishi eneo la Posta walitoka huku wakiogopa kurudi katika nyumba zao.
Katika eneo la Mwenge kwa wanafunzi wanaosoma Chuo Kikuu cha Tumaini (Tudarco) baadhi wanadaiwa kuzimia kutokana na hekaheka za tetemeko.
Tetemeko la ardhi limepita katika maeneo mbalimbali ya mikoa ya Dar es salaam ,Pwani ,Morogoro na Arusha muda mfupi uliopita na kuibua hisia kwa wakazi.
Mjiolojia Gabriel Mbogoni amesema bado hawajasoma kwenye mfumo kujua ni la kiwango gani.
Baki nasi kufahamu zaidi. pic.twitter.com/vy0tOpEXd9
— ITV (@ITVTANZANIA) August 12, 2020
Tetemeko la ardhi lenye kipimo cha 5.9 limeripotiwa jiji la Dar es Salaam na pwani ya Kenya. Hakuna madhara yoyote yaliyoripotiwa mpaka sasa #CloudsDigitalUpdates pic.twitter.com/w2BX7DHQUS
— Clouds Media (@CloudsMediaLive) August 12, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/08/12/tetemeko-la-ardhi-lapita-mikoani-ikiwemo-dar-es-salaam/
No comments:
Post a Comment