Arteta ana mpango wa kupata fedha za kuwasaini wachezaji wapya wenye makali zaidi. Picha: Hisani
Arteta ana mpango wa kuwauza zaidi ya wachezaji tisa kabla ya msimu ujao
Hii ni baada ya Arsenal kutwaa kombe la FA kwa kuicharaza Chelsea 2-1, Wembley
Kocha huyo ana mpango wa kupata fedha za kuwasaini wachezaji wapya wenye makali zaidi
Mikel Arteta ana mipango kadha wa kadha na klabu yake ya Arsenal, hii ni baada ya kutwaa ubingwa wa ligi ya FA na kupiku Chelsea kwa mabao 2-1.
Meneja huyo aliyemridhi Unai Emery katika klabu hiyo miezi nane iliyopita amepata fahari kubwa sasa akiwa katika orodha ya mameneja walioweza kutwaa taji.
Ushindi wao katika FA sasa unaipa klabu hiyo nafasi ya kushiriki katika ligi ya Uropa msimu ujao, Arteta akianza kujipanga na mapema.
Mikel Arteta to Arsenal club doctor Gary O’Driscoll after the FA Cup final win: “I told you, I told you. Believe in me, my friend. Believe in me.”
Arteta reportedly convinced O’Driscoll to stay at the club after initially agreeing to join Liverpool. #afc pic.twitter.com/kv0oUgL3NA
— afcstuff (@afcstuff) August 3, 2020
Kulingana na ripoti ya SunSports, Arteta ana mpango wa kuwauza zaidi ya wachezaji wake tisa kama njia ya kupata fedha za kuipanga vyema timu yake kwa wachezaji wenye ujuzi zaidi.
Jarida hilo limebaini kuwa bajeti ya Arteta imepanda kwa £30 milioni baada ya kutwaa ligi ya FA kwa kuipa adabu Chelsea.
Cédric Soares & Pablo Marí have played a combined 454 minutes since arriving.
This means that Mikel Arteta has essentially beaten each of this season’s top 4 with Unai Emery’s squad. pic.twitter.com/aqHlBS44DC
— Patrick Timmons (@PatrickTimmons1) August 3, 2020
Aidha, chapisho hilo limebaini kuwa wachezaji watatu kati ya timu iliyopiga Chelsea wapo kwenye orodha ya mauzo.
Alexandre Lacazette anadaiwa kuongoza katika orodha hiyo ya wachezaji wanaogura Arsenal.
Shkodran had a successful small procedure to his right hamstring on Saturday. He is aiming to return to full training in October.
Full update on @MustafiOfficial
— Arsenal (@Arsenal) July 28, 2020
Wengine wanaodaiwa kupasha misuli moto tayari kuondoka ni pamoja na Shkodran Mustafi, Sead Kolasinac, Sokratis Papastathopoulos, Lucas Torreira, Henrikh Mkhitaryan, Matteo Guendouzi na Mesut
source http://www.bongoleo.com/2020/08/04/mikel-arteta-awataja-wachezaji-9-anaowauza-kujipanga-kwa-msimu-ujao-baada-ya-kutwaa-fa/
No comments:
Post a Comment