Waziri wa Uwekezaji, Angellah Kairuki amechukua fomu ya kugombea Ubunge jimbo la Same Magharibi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Waziri huyo amekabidhiwa fomu huyo leo na Katibu wa CCM Wilaya ya Same, Victoria Mahembe.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania ubunge wa jimbo la Buhigwe.
Naye Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa, amechukua fomu katika Wilaya ya Karagwe kutetea uwakilishi wa jimbo la Karagwe.
ANGELA KAIRUKI ACHUKUA FOMU YA UBUNGE SAME
Waziri wa Uwekezaji, Angellah Jasmine KAIRUKI akichukua Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Same Magharibi kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi leo Julai 14 , 2020.
Anayemkabidhi fomu hiyo ni Katibu wa CCM Wilaya ya Same Victoria Mahembe. pic.twitter.com/lOeuz1YjjG— Clouds Media (@CloudsMediaLive) July 14, 2020
#Uchaguzi2020 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na @ccm_tanzania kuwania Ubunge jimbo la Buhigwe. pic.twitter.com/VKVm7wIdW5
— EastAfricaRadio (@earadiofm) July 14, 2020
Waziri wa Viwanda na Biashara @innobash amechukua fomu katika Ofisi ya CCM Wilaya ya Karagwe kuchukua fomu kutetea uwakilishi wa jimbo la Karagwe katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania #TiaNia2020 pic.twitter.com/ENkDx5DHMa
— Clouds Media (@CloudsMediaLive) July 14, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/14/waziri-angela-kairuki-dk-mpango-na-bashungwa-wamechukua-fomu-leo-za-kugombea/
No comments:
Post a Comment