Watu wawili wamefariki katika ajali ya Basi la Kyela Express na kujeruhi 28 ambao kati yao watatu wapo katika hali mbaya.
Basi hilo lililokuwa likitoka Dar es Salaam kwenda Wilayani Kyela limepinduka usiku wa kuamkia leo katika njia panda ya Lutengano kijiji cha Ushirika Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, John Merina, alithibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kueleza majeruhi watatu wamekimbizwa hospitali ya rufaa ya Mbeya kwa ajili ya matibu zaidi.
#AjaliyaKyelaExpress:Mganga Mkuu wa wilaya ya Rungwe, John Merina amethibitisha vifo viwili na majeruhi 28, kati yao watatu hali zao ni mbaya na wamekimbizwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa matibabu zaidi.#ITVUpdates. pic.twitter.com/EBCK2PIdzu
— Radio One Stereo (@RadioOneStereo) July 17, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/17/watu-wawili-wamefariki-katika-ajali-ya-basi-na-kujeruhi-28/
No comments:
Post a Comment