Rais John Magufuli amesema DK. Seif Shekalagh ni daktari mwenye taaluma na amesoma akapatiwa Shahada ya Udhamivu (PHD) kutoka nchini Uholanzi na kwenda kwenye kituo cha utafiti.
“Miaka ya nyumba aliomba Ubunge Korogwe hakuwa na hela wala nini alitaka kuwatumikia wana korogwe akapigwa chini,” amesema Rais Magufuli.
“Alivyokosa ubunge akaurudi kwenye mambo yake ya utafiti alipoondoka nikasema mbona huyu anapenda siasa nikaona acha nimjaribu kidogo,” amesema Rais
Rais Magufuli amesema alimpa nafasio ya ukuu wa wilaya ya Maswa, hakukata tamaa akaenda kufanya kazi vizuri.
“Maswa ni miongoni mwa Wilaya zilizoanzisha viwanda vya mkakati ndio maana tukasema tumpandishe,” alisema Magufuli
source http://www.bongoleo.com/2020/07/20/rais-magufuli-dk-seif-alishawahi-kuomba-kugombea-ubunge-korogwe-hakuwa-na-hela-akapigwa-chini/
No comments:
Post a Comment