Kampuni maarufu inayomilikiwa na Diamond Platnamaz, Wasafi, iliandaa hafla kumshrehekea msanii mpya Zuchu
Wema na Diamond waliawaacha wengi vinywa wazi kwa densi yao katika hafla hiyo
Walinengua viuno kwa tabasamu na kumbukumbu za mapenzi yao ya zamani
Ni wazi kuwa chembe chembe za mapenzi kati ya Diamond Platnamz na Wema Sepetu zingali zipo na sherehe iliyoandaliwa na kampuni ya Wasafi imethitisha hili.
Wawili hao waliwaacha wengi vinywa wazi kwa kumbukumbu za mapenzi baada ya kujitokeza hadharani kunengua viuno pamoja na kufarahiana katika sherehe hiyo ya kukata na shoka.
Sherehe hiyo iliyopewa jina I AM ZUCHU iliandaliwa na kampuni ya Wasafi kusherekea hatua aliyopiza Zuchu katika safari yake usanii.
Hafla hiyo iliandaliwa Jumamosi, Julai 18 Mlimani Hall Tanzania wapenzi hao wawili wa zamani hawakuchelea kuipa kilele kwa densi yao maridadi.
Mbosso alipopanda jukwani kupiga kibao chake hodari wa mapenzi, mahodari wa mapenzi, Wema na Diamond waliamka na kuuonyesha ulimwengu maana kamili ya mapenzi.
Wengi waliwashangilia huku densi ya ikishika kasi wakionyesha furaha kwa tabasamu la aina yake.
Haya yanajiri tu miezi mitano baada ya Diamond na Tanasha Donna kuosnyeshana visogo.
Diamond alijitokeza siku chache zilizopita na kueleza kuwa ashapata mpenzi mwengine na kuwa mipango ya kumfungisha pingu za maisha i njiani.
source http://www.bongoleo.com/2020/07/20/diamond-na-wema-sepetu-watesa-mitandao-wa-densi-ya-mapenzi-wanarudiana/
No comments:
Post a Comment