Rais John Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi wa mikoa na wilaya na kumteua Abubakar Kunenge kuwa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam.
Kabla ya uteuzi huo Kunenga alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam na anachukua nafasi ya Paul Makonda.
Rais Magufuli amemteua Joseph Joseph Mkirikiti kuwa mkuu wa mkoa Manyara . Kabla ya uteuzi huo Mkirikiti alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang mkoani Manyara na anachukua nafasi ya Alexander Mnyeti.
Rais Magufuli amemteua Paulo Mshimo Makanza kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam.
Kabla ya uteuzi huo Makanza alikuwa Ofisa Mwandamizi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) anakwenda kuchukua nafasi ya Aboubakar Kunenge ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Rais Magufuli amemteua Dk. Seleman Serera kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma.
Kabla ya uteuzi huo Dk Serera alikuwa Ofisa Mwandamiza wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Makao Makuu na anachukua nafasi ya Deo Ndejembi.
U T E U Z I.
Wakuu wa Mikoa
Katibu Tawala wa Mkoa
Wakuu wa Wilaya
Wakurugenzi wa Halmashauri
Makatibu Tawal wa Wilaya pic.twitter.com/48HNJiLc0d— Gerson Msigwa (@MsigwaGerson) July 15, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/15/rais-magufuli-awatumbua-wakuu-wa-mikoa-akiwemo-makonda/
No comments:
Post a Comment