Rais John Magufuli amefanya uteuzi kwa viongozi mbalimbali huku akimteua Dk. Jumanne Fhika kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
Kabla ya uteuzi huo, Dk. Fhika alikuwa ofisi ya Rais na anachukua nafasi ya Christopher Ole Sendeka.
Rais amemteua DK. Aloyce Nzuki kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii.
Kabla ya uteuzi huo Dk Nzuki alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii anakwenda kuchukua nafasi ya Prof. Adolf Mkenda.
Rais Magufuli amemteua mhandisi Anthony Sanga kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maji.
Kabla ya uteuzi huo mhandisi Sanga alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji anaenda kuchukua nafasi ya Profesa Kitila Mkumbo.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dk Allan Kijazi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili.
RUKSA na FURSA.
JPM afanya uteuzi wa RC, KM, NKM na DC. pic.twitter.com/UZBZN8ExxF
— Gerson Msigwa (@MsigwaGerson) July 17, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/17/rais-magufuli-amtumbua-ole-sendeka-katambi-na-makatibu-wakuu-wa-wizara/
No comments:
Post a Comment