Wapelelezi wameeleza kuwa mwanamke huyo alipokonywa bastola baada ya kisa
Alivalia sare za dereva wa kampuni FedEx wakati wa kisa
Haijabainika ni kwanini aliamua kuchukua hatua hiyo
Jaji mmoja raia wa Amerika amewaacha wengi kwa mshangao baada ya kumuua mwanawe mwenye umri wa miaka 20 kwa kumpiga risasi kabla kumgeukia mumewe na kummiminia risasi vile vile.
Kwa mujibu wa vyombo vy habari vya US, Esther Salas alifika myumbani kwake mwendo wa 5pm Jumapili, Julai 19 akiwa amevalia sare za madereva wa FedEx na kuanza kumfyatulia risasi na kumuua mwanawe Daniel Anderl kabal kumgeukia mumewe, Mark Ander na kumjeruhi vibaya kwa risasi.
Akizungumza na jarida la ABC, meya Francis Womack alisema kuwa jaji huyo alikuwa anatishiwa suala ambalo limefutiliwa mbali na majirani wake.
Alivalia sare za dereva wa kampuni FedEx wakati wa kisa. Picha:Hisani.
Wajasusi wa FBI tayari wameanza msako mkali kumtafuta jaji huyo aliyetoweka baada ya kufanya unyama huo. Wametoa wito kwa umma kutoa habari zozote kuhusiana na kisa hicho.
‘’ Tunashirikiana kwa karibu na wenyeji wa hapa na tutatoa habari zaidi wakati ufaao.’’ Walisema.
Seneta wa jimbo la New Jersey Bob Menendez ameshangazwa na kisa hicho na kutaka waliohusika kivyovyote katika kisa hicho kuchukuliwa hatu upesi.
‘’ Namjua vizuri Jaji Salas pamoja na mumewe, na nilikuwa furaha kumpendekeza kwa Obama kwa uteuzi katika kamati aliyofanyakazi kama jaji mwenye tajriba mkubwa.’’ Jersey Bob alisema.
source http://www.bongoleo.com/2020/07/20/jaji-maarufu-amuua-mwanawe-kinyama-amjeruhi-vibaya-mumewe-kwa-risasi/
No comments:
Post a Comment