Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole, amesema sifa mojawapo ya kiongozi wa CCM ni kutosheka.
“Ukiambiwa umepata sema asante na ukiambiwa umekosa pia unasema asante,” alisema Polepole.
Polepole alisema kuna watu wameteuliwa na Rais John Magufuli tangu mwaka 2015 na kwa sasa wamefikia kwenye mto wanaondoka.
“Chama hiki kikipata viongozi wasiotosheka ni shida, mtu asiyetosheka ukimpa kazi hii atakuacha mtoni, ukimpa nyingine atakuacha mtoni. Tukifika kwenye chama kule tutaangalia kama alituvusha kwenye mto ama hakutuvusha,”
"Sifa moja ya kiongozi wa CCM ni kutosheka, ukiambiwa umepata sema asante na ukiambiwa umekosa pia unasema asante. Kuna watu wameteuliwa na Rais Magufuli tangu 2015 lakni sasa wamefika kwenye mto wanaondoka" – @hpolepole #MkutanoCCMRuvuma pic.twitter.com/HVNHxAdIhz
— EastAfricaRadio (@earadiofm) July 18, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/18/polepole-tukipata-viongozi-wasiotosheka-ni-shida-atakuacha-mtoni-tutawaangalia-kama-alituvusha/
No comments:
Post a Comment