Aliyekuwa mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, amesema kugombea kupitia upinzani ni maisha ya roho mkononi kila wakati.
Amesema unaweza kufutiwa uraia, kubambikiwa kesi, kufilisiwa, kutekwa, kujeruhiliwa, kuuawa na kuteswa kisaikolojia.
Lema aliandika ujumbe huo katika ukurasa wake wa Twitter kuwa ” Ni utitiri wa visa na hofu,”.
“Unashika fomu ya kugombea mkono mmoja na mkono wa pili unaandika wosia,” aliandika Lema.
Kugombea kupitia upinzani ni maisha ya roho mkononi kila wakati. Kufutiwa uraia, kubambikiwa kesi, kufilisiwa, kutekwa, kujeruhiwa, kuuawa, na kuteswa kisaikolojia. Ni utitiri wa visa na hofu. Unashika fomu ya kugombea mkono mmoja na mkono wa pili unaandika wosia.
— Godbless E.J. Lema (@godbless_lema) July 15, 2020
source http://www.bongoleo.com/2020/07/15/lema-kugombea-kupitia-upinzani-ujiandae-kufutiwa-uraia-kutekwa-ama-kubambikiwa-kesi/
No comments:
Post a Comment