Kilikuwa kisa cha kutamausha baada ya habari kuenea kuwa bibi harusi huyo alifariki
Katika baadhi ya picha za harusi mtandaoni, imebainika kuwa mwanadada alitoka hospitalini kufanya harusi hiyo
Mapenzi ni kitu cha ajabu sana na mara nyingi si rahisi kukielewa. Huku wengi wakisema kuwa mapenzi hayana macho, naamini kila anayejihusisha hujihoji kikamilifu kabla kujitumbukiza kwayo.
Naam, mapenzi ya kweli yapo, na iwapo huamini, pia hutaamini kuhusu kisa cha Vivian, bibi harusi raia wa Nigeria aliyefariki siku moja tu baada ya kufunga pingu za maisha.
Vivian na mpenziwe wa dhati walifunga pingu za maisha Jumamosi, Julai 17 kwa harusi ya kukata na shoka na kuonyeshana mapenzi ya kweli bila kujali mapungufu yao.
Harusi yao ilikuwa himizo kwa wengi maana bibi harusi alionekana akiwa mgonjwa na kuwa hata wakati wa harusi, alikuwa ametoka hospitalini kuungana na mumewe katika sherehe hiyo, sindano mkononi ikiwa thibitisho.
UPDATE 20/07/2020The face of the Lady wey do wedding on Saturday and die on Sunday. Maybe she nor dey medically fit…
Posted by Sapele Oghenek on Monday, 20 July 2020
Badala ya kutoa gari na mali za dunia, mume huyo alikuwa tayari kutoa maisha yake kwa mkewe aliyekuwa akiugua kumuonyesha mapenzi makuu aliyokuwa nayo kwake.
Harusi ilinoga lakini la kutamausha ni kuwa bibi harusi huyo alifariki Jumapili, Julai 19, siku moja tu baada ya harusi hiyo.
If you know you would leave us this soon, why did you allow me to put on Asoebi for you
Posted by Efenadju Bernice on Monday, 20 July 2020
Hadi sasa haijabainika alichokuwa akiuguza bibi harusi huyo, wengi wakijimwaya mitandaini kutuma jumbe za rambi rambi kwa jamaa na marafiki.
source http://www.bongoleo.com/2020/07/21/kisa-cha-bi-harusi-aliyefariki-saa-chache-baada-ya-harusi-yake/
No comments:
Post a Comment