Wednesday, July 15, 2020

Dondoo za leo: Zitto asema Sheikh Ponda haonekani vituo vya Polisi, Mume amuua mkewe kwa kumchinja na yeye kujinyonga na Matokeo kura za maoni Chadema yashtua wengi

Habari ya asubuhi mdau wa Opera News ni siku nyingine ya Alhamisi Julai 16, 2020, matumaini yetu upo salama na karibu katika ujenzi wa taifa.

Tunakukaribusha katika dawati letu la dondoo tupate kukujuza habari tatu zinazopamba asubuhi ya leo.

Habari hizo ni Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asema Sheikh Ponda haonekani kwenye vituo vya polisi kulikoni? Mume amuua mkewe kwa kumchinja shingoni na yeye kujinyonga je unajua chanzo cha kutokea mauaji hayo ni nini? soma habari hii kwa kina na matokeo kura za maoni Chadema yashtua wengi.

Karibu msomaji wetu;

ZITTO: NIMEJULISHWA NA MAWAKILI SHEIKH PONDA HAONEKANI KATIKA VITUO VYA POLISI

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema amejulishwa na mawakili kuwa Sheikh Ponda Issa Ponda haonekani kwenye vituo vyote vya polisi jijini Dar es Salaam.

“Pamoja na juhudi zinazofanywa na mawakili kuhakikisha kuwa anafikishwa mahakamani,” aliandika Zitto katika ukurasa wake wa twitter.

Zitto amelitaka jeshi la polisi  kumuachia huru mara moja Sheikh Ponda na kwamba wanatakiwa kutenda haki.

Soma zaidi

MUME AMUUA MKEWE KWA KUMCHINJA SHINGONI NA YEYE KUJINYONGA

Mkazi wa Kijiji cha Mipanga Kata ya Maji Moto Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi, Dalali Malongo (20) ameuawa kikatili kwa kuchinjwa shingo na mume wake aitwaye, Kisabo  Joseph baaada ya mume wake kukasirishwa na kitendo cha mke wake kumnyima tendo la ndoa kwa muda mrefu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Benjamin Kuzaga amesema tukio hilo la mauaji lilitokea Julai 14, mwaka huu majira ya saa moja jioni Kijiji cha Mipanga Kata ya Maji Moto Wilaya ya Mlele.

Amesema marehemu na mtuhumiwa walikuwa ni wanandoa waliokuwa wakiishi pamoja kama mume na mke.

Soma zaidi

MATOKEO KURA ZA MAONI CHADEMA YASHTUA WENGI

MMATOKEO  ya kura za maoni ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), yameendelea kushtua kutokana na makada wanawake wa chama hicho kuibuka washindi katika maeneo mengi.

Katika kura hizo zilizoanza kupigwa mwanzoni mwa wiki, wabunge waliomaliza muda wao katika Bunge lililopita kupitia chama hicho, wameibuka washindi.

Kwa matokeo yaliyotangazwa jana, waliong`ara katika kura za maoni ni Lucy Owenya (Moshi Vijijini) ambaye pia ameshinda kwenye kipengele cha ubunge viti maalum kwenye jimbo hilo hilo.

Soma zaidi



source http://www.bongoleo.com/2020/07/16/dondoo-za-leo-zitto-asema-sheikh-ponda-haonekani-vituo-vya-polisi-mume-amuua-mkewe-kwa-kumchinja-na-yeye-kujinyonga-na-matokeo-kura-za-maoni-chadema-yashtua-wengi/

No comments:

Post a Comment