Thursday, July 23, 2020

Bodi Ya Mikopo Yatoa Ufafanuzi Wanafunzi Kupunguziwa Fedha

HESLB | WebBaada ya sakata la wanafunzi wa vyuo mbalimbali nchini kulalamika kupunguziwa pesa za kujikimu na bodi ya mikopo kuliko ilivyo kawaida ya pesa wanapewa kila mwezi kama sehemu ya kujikimu wanapokuwa masomoni.

Leo Juali 23, 2020 bodi ya mikopo nchini imetoa ufafanuzi juu ya hali ilivyo kwa wanafunzi walilalamika kupunguziwa pesa za kujikimu kwenye kipindi cha miezi kadha ailiyosalia cha kukaa chuoni.

“Malengo ya fedha hizi ni kunufaisha wanafunzi ili kuongeza wasomi wengi nchini, pesa zinalipwa kulingana na muongozo na ratiba ya chuo husika, kama chuo kikisema utakaa chuo kwa siku ishirini utapatiwa pesa ya siku ishirini bila upungufu wowote, lakini kinachotokea hapa ni mwanafunzi anataka alipwe hadi muda ambao yuko likizo”amesema mkuu wa kitengo cha  Mwasiliano Omega Ngole.

View this post on Instagram

HESLB: HATUJAPUNGUZA MIKOPO. TUNATOA FEDHA ZA KUJIKIMU KULINGANA NA SIKU ZA MASOMO – Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imefafanua kuwa inatoa mkopo kwa Wanafunzi kulingana na siku za masomo kwa kila robo ya mwaka wa masomo – Imeeleza kuwa kutokana na #COVID19 siku za masomo za robo mwaka ya nne ya muhula wa masomo wa 2019/20 ambazo huwa ni 60 zimepungua kwa baadhi ya Vyuo ambapo baadhi vyuo vimebakiwa na siku 45 za masomo – Imesisitiza kuwa Wanafunzi watakaosaini wataona kwenye nyaraka zao kuwa fedha zimepungua kulingana na siku za masomo watakazokuwa nazo kuanzia Agosti 01 – Aidha, Bodi imeongeza kuwa kuhusu kuwaarifu Wanafunzi juu ya suala hilo, wao wanaongea na Chuo kwa maana taarifa za Wanafunzi wanaosoma ikiwemo matokeo wanapewa na Chuo husika. Pia, mabadiliko yoyote hufanyika ndani ya Mabaraza ambayo Viongozi wa Wanafunzi wanakuwepo – Kuhusu ada kulipwa yote bila kukatwa, Bodi imeeleza kuwa siku za masomo zimepungua ila muda wa masomo kwa siku umeongezeka kufidia siku zilizopungua na kufanya walimu kuendelea kufundisha kwa jumla ile ile ya saa kama ambavyo siku zingekuwa hazijapungua #JamiiForums #HESLB #Wanafunzi

A post shared by JamiiForums (@jamiiforums) on



source http://www.bongoleo.com/2020/07/23/bodi-ya-mikopo-yatoa-ufafanuzi-wanafunzi-kupunguziwa-fedha/

No comments:

Post a Comment