Friday, July 31, 2020

Tanzania yaifungia Kenya kuleta ndege zake nchini

Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imefuta kibai kilichokuwa kinarusha ndege za Shirika la Ndege la Kenya (KQ) kutua Tanzania.

Uamuzi huo umekuja baada ya Kenya kutoiweka Tanzania katika orodha ya nchi ambazo raia wake wataruhusiwa kuingia Kenya kuanzia Agosti 01, 2020.

Kwa mujibu wa taarifa iiyotowa jana kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari, ameeeza Kenya wametangaza kuwa Agosti 01, 2020 kufungua anga lake kwa usafiri wa  ndege za kimataifa kuanza kuingia nchini Kenya tangu walivyozuia Marchi 25, 2020.

Hamza Johari

Taarifa hiyo imeeleza kuwa ndege ya Kenya (KQ) inayofanya safari zake  Dar es Saaam, Kilimanjaro na Zanzibar hazitakiwi kuingia Tanzania kutokana na notisi waliyoitoa mpaka watakapotangaza tena.



source http://www.bongoleo.com/2020/08/01/tanzania-yaifungia-kenya-kuleta-ndege-zake-nchini/

Kinachojiri kwenye magazeti ya leo Agosti 01, 2020

Habari mdau wetu leo ni Jumamosi ya Agosti 01, 2020 tunakukaribisha utazame kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma za magazeti  ya nchini.

Kipengele hiki Muhimu katika kuhabarika na Opera News kinapatikana kila siku asubuhi.

Kwa ujumla yapo magazeti mbalimbali yaliyosheheni habari za kisiasa, burudani, michezo na  elimu.

Habari kubwa zilizosheheni kwenye kurasa za mbele za magazeti ya leo, karibu msomaji wetu ujisomee.

   

 

 

 

HARMONIZE KAMTANGAZA MSANII MPYA KONDE GANG ANATOKEA NIGERIA



source http://www.bongoleo.com/2020/08/01/kinachojiri-kwenye-magazeti-ya-leo-agosti-01-2020/

Bingwa wa Ndondi Mayweather kurudi Uwanjani Baada ya Kustaafu, Uhondo Kamili

Floyd Mayweather: Khan claims ex-boxer will come out of retirement because he's broke

Huenda Mayweather atarejea uwanjani mwaka huu

Bingwa huyo wa ndondi anadaiwa kumaliza hela zote alizowehifadhi

Mwanandondi mwenza Amir Khan ametoa madai hayo

Aliyekuwa nyota wa ndondi Floyd Mayweather atarejea uwanjani mwaka huu kwa mara ya kwanza tangu alipostaafu 2017, hii ni kulingana na mwanandondo mwenza Amir Khan.

Mayweather aliyestaafu 2017 akiwa na umri wa miaka 40 anadaiwa kuchukua hatua ya kurejea kwenye uwanja baada ya kufyonza fedha zote alizowekeza huku sasa umaskini ukimkodolea macho.

Floyd alitengeneza mabilioni ya pesa baada ya kuibuka mshindi kwa takriban mechi 50 alizoshiriki mtawalia na kuibuka mshindi.

‘’ Floyd Mayweather ni kati ya wale ambao huenda wamemazliza hela zao na watalazimka kurudi uwanjani,’’ Amir Khan alisema.

Anatumia hela nyingi sana, ila sijui kama atapenda wazo hilo la kurudi uwanjani. Kama nilivyosema, huenda atarudi,’’ aliongezea.

Inadaiwa kuwa Floyd alikuwa akipata mshahara mrefu wa  $1 bilioni lakini Mc Gregor pamoja na aliyekuwa rafikiye wa karibu 50 Cent alifyonza hela hizo zote.

Iwapo atarudi uwanjani, Mayweather ataibua kibarua kigumu kwa wanandondi wenza maana hamna aliyefanikiwa kumpiku katika mchezo huo.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/bingwa-wa-ndondi-mayweather-kurudi-uwanjani-baada-ya-kustaafu-uhondo-kamili/

Mbwa wa Kwanza aliyepatikana na COVID19 Afariki Amerika

Buddy: First dog to test positive for COVID-19 in the US dies

Buddy alipatakana na corona Mei 2020 baada ya kuanza kuugua tangu Aprili 2020

Indaiwa kuwa mbwa huyo aliambukizwa virusi hivyo na mmiliki wake

Mmiliki huyo alieleza kuwa mbya huyo alianza kudhoofika na kutapika damu iliyoganda

Mbwa aina ya German Shepard mwenye umri wa miaka saba aliyekuwa wa knwa kupatikana na virusi vya covid19 amefariki, New York.

Mbwa huyo aliyepewa jina Buddy alifariki Jumamosi, Julai 11 baada ya kuugua kwa miezi mitatu.

Kulingana jarida la CNN, madaktari wa mifigo waliochunguza ripoti ya mbwa huyo walielza kuwa alikuwa akiugua saratani.

‘’ Haibainiki iwapo saratani ilimfanya kuambukizwa kwa urahisi na virusi vya corona, ama huenda ilikuwa ni sadfa tu.

Mbwa huyo alianza kuugua Aprili 2020, mmiliki wake Robert Mahomey alimshuku kuambukizwa virusi vya corona, alipomuita daktari wa mifugo, alifanya vipimo na kuthibitishwa kuwa kweli alikuwa na virusi hivyo.

Juni, 2, 2020, kitengo cha kilimo USDA kilithibitisha kuwa Buddy alikuwa mbwa wa kwanza kuambukizwa covid19.

USDA hadi sasa imethibitisha idadi ya takriban mbwa 12 na paka 10 walioambukizwa corona.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/mbwa-wa-kwanza-aliyepatikana-na-covid19-afariki-amerika/

Waziri Kamwelwe amtumbua Meneja wa Tanroads

 

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, ametengua nafasi ya Meneje wa Wakala wa Barabara (Tanroads) mkoa wa Lindi, Mhandisi Isack Mwanawima.

Waziri Kamwelwe ametoa taarifa hiyo jana kwa vyombo vyake habari kuhusiana na kumsimamisha kazi Meneja huyo.

Amesema jana Rais John Magufuli akiwa anatokea kijiji cha Lupaso katika mazishi ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, ameshuhudia ubovu mkubwa wa barabara kipande cha Nangurukuru hadi Mbwemkuru yenye urefu wa kilometa 90.

“Kwa kuwa nilishawahi kutoa maelekezo kwa mameneja wa mkoa wa Tanroads kuhakikisha barabara wanazosimamia zinakuwa kwenye hali nzuri na zinapitika,” taarifa hiyo ilieleza.

Amesema kutokana na uzaifu huo ametengua nafasi ya meneja huyo na kumuagiza Mtendaji Mkuu wa Tanroads apeleke mhandisi mwingine haraka kwa ajili ya kuimarisha usimamizi na kufanya maboresho ya Barbara hiyo.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/waziri-kamwelwe-amtumbua-meneja-wa-tanroads/

Rais wa Gambia Atiwa Karantini, Naibu Wake Apatikana na COVID19

Adama Barrow: Gambia haitojiondoa ICC

Adama atajitenga humo kwa wiki mbili. Picha: Hisani

Rais wa Gambia Adama Barrow ameingizwa karantini baada ya naibu wake kupatikana na virusi vya corona

Kulingana na taarifa ya ikulu, Adama atajitenga humo kwa wiki mbili

Virusi vya corona vimezidi kuunguza mataifa bila huruma hata baada ya masharti makali kuwekwa kama njia ya kujikinga.

Virusi hivyo vikitekeza bila kujali tabaka, hali na mali, viongozi wa mataifa mbali mbali wameambukizwa virusi hivyo bila kuwaacha wananchi wa kawaida.

Awamu hii, virusi hivyo vimetikisa Gambia. Rais wa nchi hiyo Adama Barrow akichukua hatua ya kujitenga kwenye karantini baada ya naibu wake kupatikana na virusi hivyo hatari.

Kwa mujibu wa ikulu ya nchi hiyo, Barrow atasali karantini kwa wiki mbili huku madaktari wake wakimchunguza kwa karibu.

Rais huyo aliamua kujitia karantini baada ya kutangamana na naibu wake ambaye pia alipatikana na virusi hivyo.

Hadi sasa, Gambia imerekodi vsa 326 vya maambukiza ya corona pamoja na vifo nane.

Serikali imesisitiza kuhusu kufuatwa kwa kanuni za wizara ya afya katika kujikinga na virusi hiyo hatari.

Kwingineko, mkewe Rais wa Brazil Michelle Bolsanaro pia amethibitishwa kuambukizwa virusi vya corona.

Kulingana na vyombo vya habari nchini humo, Michelle alipatikana na virusi vya corona Julai 30, siku moja tu baada ya kuhudhuria mkutano wa hadhara akiandamana na mumewe.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/rais-wa-gambia-atiwa-karantini-naibu-wake-apatikana-na-covid19/

Takukuru inamshikilia mfanyabiashara Alute kwa kufanya utapeli wa nyumba na viwanja

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Manyara inamshikilia Japhet Samweli Alute kwa kufanya biashara ya mikopo umiza inayoambatana na kukopesha wananchi kwa ribs kubwa na kisha kuwadhulumu mali zao wanazo weka kama dhamana.

Alute anafanya biashara hiyo bima kuwa na leseni ya biashara, jambo ambalo linaikosesha serikali mapato kutokana na ukwepaji kodi.

Biashara ya fedha inatakiwa kupatiwa kibali cha Benki Kuu (BoT) jambo ambalo hakulitekeleza na hana leseni ya biashara.

Alute anatumia jina la Halmashauri ya mji wa Babati kuwatishia wananchi wanaochelewesha kufanya marejesho kwa kuwatumia ujumbe wa kuwauzia maeneo yao au nyumba walizoweka kama dhamana kwa mikopo umiza.

Mtuhumiwa huyo amepekuliwa na kupatikana na mikataba ya kitapeli 99 ambayo inaonyesha ameuza maeneo mbalimbali zikiwemo nyumba na viwanja vya wananchi Babati.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/takukuru-inamshikilia-mfanyabiashara-alute-kwa-kufanya-utapeli-wa-nyumba-na-viwanja/

Jamaa aliyemuua Nyani Uganda Afungwa Miaka 11 Gerezani

Rafiki

Aina hiyo ya nyani (Mountain gorillas) ni nadra mno. Picha:Hisani

Felix Byamukama alikiri kumuua nyani huyo

Alileza kuwa nyani huyo alimvamia ndipo akaamua kumuua kama njia ya kujikinga

Bwana mmoja raia wa Uganda atalazimika kutumikia kifungo cha miaka 11 jela baada ya kupatikana na hatia kwa kumuua nyani kinyume cha sheria.

Akizungumza mbele ya hakimu, Felix Byamukama alikiri kuingia kwenye mbuga la wanyama na kumuua nyani huyo aliyetambulika kama Rafiki.

Byamukama alidai kuwa alimuua Rafiki kama njia ya kujikinga baada ya nyani huyo kumvamia mbugani humo. Kando na hivyo, alikiri kuingia kwenye mbuga hilo la Bwindi kwa lengo la kuwawinda wanyama wadogo na wala si kwa nia ya kumuua nyani huyo.

Uchunguzi ulibaini kuwa Rafiki alifariki kutokana na kudungwa sehemu za ndani kwa kifaa chenye makali.

Rafiki eating something

Nyani huyo alitoweka Juni 1, na mwili wake kupatikana siku moja baadaye. Picha: Hisani

Kwa mujijibu wa jarida la BBC, maafisa ya UWA, kitengo kinachosimamia wanyama pori walimtafuta muuaji huyo na kumpata kijijini akiwa na silaha za uwindaji.

Nyani huyo anadhaniwa na kuwa na umri wa miaka 25,akiwa ni aina moja ya nyani ambayo huwa nadra sana.

Rafiki alikuwa rafiki mkuu wa wanadamu na kila watalii walipofika mbugani, aliwapa upendo mkubwa kwa kutangamana nao na kutembea nao kila mahali.

Inadaiwa kuwa mwindaji huyo alipoingia mbugani, huenda nyani huyo alidhania ni mtalii na kama kawaida alitaka kutangamana naye na katika hali hiyo akauliwa.

Mbuga zimefungwa kwa muda tangu kulipuka kwa virusi vya corona.

 



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/jamaa-aliyemuua-nyani-uganda-afungwa-miaka-11-gerezani/

Fatma Karume amelicharua jeshi la polisi na kuwaambia tusitishane kabisa

Wakili wa kujitegemea, Fatma Karume amesema alilalamika kuhusu jengo lake kupigwa bomu na hakuna majibu yoyote aliyopewa hadi sasa.

Jana jeshi la polisi limemtaka mtu yoyote ambaye anahofu na usalama wake kutoa taarifa hizo polii ili ziweze kufanyiwa kazi badala ya kulalamika mitandaoni na kwenye vyombo vya habari vya ndani na nje.

“Mimi nimelalamika kuhusu jengo langu kupigwa bomu. Nimeenda mpaka kwa DCI pale HQ Wizara ya ndani @ tanpol mpaka hii leo hamjanipa majibu yoyote,” aliandika Fatma katika ukurasa wake wa twitter

“Bado mnataka nikae kimya ili iweje? nitalalamika tu kwamba hamjanipatia majibu yeyote wala hamjakamata mtu. tusitishane kabisa,”

Fatma aliendelea kusema kuwa “Eti mpige mabomu majengo ya watu mpige risasi wenzake, mchoma visu wenzake, mtekaji na @tanpol wanaoshindwa kuwakamata si wachafu nchi, alkini sisi Victims tunaolalamika eti tunaichafua nchi? wekeni sheria ya kufunga walalamikaji badala ya wahalifu msitufanye wapumbavu,”.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/fatma-karume-amelicharua-jeshi-la-polisi-na-kuwaambia-tusitishane-kabisa/

Mke wa Rais wa Brazil Aambukizwa Covid19

Brazil first lady, another Cabinet minister infected | CTV News

Mkewe Rais wa Brazil Jiar Bolsonaro amepatikana na virusi vya corona, hii ni kwa mujibu wa taarifa ya ikulu

Habari kuhusu kuambukizwa kwake yanajiri siku chache tu baada Rais huyo kupona

Virusi vya corona vimetikisa nchi ya Brazil kwa mara nyingine, wakati huu mkewe Jiar Bolsonaro rais wa nchi hiyo akitangazwa kuugua virusi hivyo hatari.

Ripoti kuhusu kuambukizwa  kwa Michelle Bolsonaro inajiri siku chache tu baada ya mumewe aliyeammbukizwa vile vile kutangaza kuwa amepata afueni.

Kulingana na taarifa kutoka ikulu, licha ya kuambukizwa virusi hivyo, Michelle yuko katika hali imara na kuwa madaktari wa ikulu wanafanya kila nia kuhakikisha anapona upesi.

What is coronavirus? COVID-19 explained - CNN

‘’ Hali yake iko imara na tunafuatilia kila kitu kwa karibu,’’idara ya habari na mawasiliano katika ikulu ilitaarifu.

Kulingana na vyombo vya habari nchini humo, Michelle alipatikana na virusi vya corona Julai 30, siku moja tu baada ya kuhudhuria mkutano wa hadhara akiandamana na mumewe.

Akihudhuria mkutano huo, Michelle na mumewe walionekana wakiwa wamevalia barakoa kama njia ya kujikinga.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/mke-wa-rais-wa-brazil-aambukizwa-covid19/

Dondoo za leo: Watu 10 wamefariki na 100 waokolewa, Kesi ya Lissu na mustakabaliwake katika safari ya Urais na Shahidi aeleza Diwani wa CCM alivyopokea rushwa

Habari ya asubuhi mdau wa Opera News ni siku nyingine ya Ijumaa Julai 31, 2020, matumaini yetu upo salama na karibu katika ujenzi wa taifa.

Tunakukaribusha katika dawati letu la dondoo tupate kukujuza habari tatu zinazopamba asubuhi ya leo.

Habari hizo ni Watu 10 wamefariki na wengine 100 kuokolewa katika ajali ya boti mkoani Kigoma, Kesi ya Lissu na mustakabali wake katika safari ya kuusaka Urais na Shahidi aeleza Diwani wa CCM alivyopokea rushwa na kukamatwa.

WATU 10 WAMEFARIKI NA WENGINE 100 KUOKOLEWA

Watu 10 wamefariki dunia na wengine 100 wameokolewa baada ya boti waliyosafiri nayo kupatwa dhoruba na kuzama katika ziwa Tanganyika.

Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye amethibitisha kutokea kwa tukio.

Soma zaidi

KESI DHIDI YA LISSU, MUSTAKABALI WAKE KATIKA SAFARI YA URAIS

Siku chache baada ya kuwasili nchini Tanzania akitokea kwenye matibabu huko Ubelgiji na kulakiwa na maelfu ya wafuasi na wanachama wa Chadema, mwanasiasa Tundu Lissu ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ameanza kuonja joto la kesi zinazomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini Dar es salaam.

Suala hili limeibua hisia tofauti kuhusu hatima ya kiongozi huyo katika kinya’ng’anyiro cha urais ndani ya chama, muungano mwaka huu wa 2020 na siasa kwa ujumla, licha ya haki zake kulindwa na katiba kwa vile hajawahi kutiwa hatiani kati ya tuhuma zilizomkabili kwa kipindi cha miaka mitano.

Soma zaidi

SHAHIDI AELEZA DIWANI WA CCM ALIVYOPOKEA RUSHWA

SHAHIDI wa kwanza Yusufu Shaban Omar Matimbwa katika kesi inayomkabili Diwani wa Kijichi, Mbagala jijini Dar es Salaam Elias Mtarawanje (29), anayedaiwa kupokea rushwa, ameeleza namna Polisi walivyoweka mtego na kufanikiwa kumnasa kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Shahidi huyo ambaye ni mwekezaji wa Hotel ya Giraffe Temeke jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi tarehe 30 Julai 2020 amedai ana ushahidi wa kutosha kuithibitisha mahakama kuwa Diwani huyo alipokea rushwa ya sh milioni moja za mtego kutoka kwake.

Diwani Mtarawanji alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke mwaka huu, akikabiliwa na mashtaka mawili likiwamo la kupokea rushwa ya Sh. 1 milioni kutoka kwa Matimbwa.

Soma zaidi

 

 



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/dondoo-za-leo-watu-10-wamefariki-na-100-waokolewa-kesi-ya-lissu-na-mustakabaliwake-katika-safari-ya-urais-na-shahidi-aeleza-diwani-wa-ccm-alivyopokea-rushwa/

Thursday, July 30, 2020

Watu 10 wamefariki dunia na wengine 87 wameokolewa mkoani Kigoma

Watu 10 wamefariki dunia na wengine 87 wameokolewa baada ya boti waliyosafiri nayo kupitwa dhoriba na kuzama katika ziwa Tanganyika.

Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye amethibitisha kutokea kwa tukio.

https://twitter.com/earadiofm/status/1289074331885154304?s=08

Tutaendelea kukupatia taarifa nyingine kuhuhusiana na tukio hilo hapo baadaye.



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/watu-10-wamefariki-dunia-na-wengine-87-wameokolewa-mkoani-kigoma/

Kinachojiri kwenye magazeti ya leo Julai 31, 2002

Habari mdau wetu leo ni Ijumaa ya Julai 31, 2020 tunakukaribisha utazame kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma za magazeti  ya nchini.

Kipengele hiki Muhimu katika kuhabarika na Opera News kinapatikana kila siku asubuhi.

Kwa ujumla yapo magazeti mbalimbali yaliyosheheni habari za kisiasa, burudani, michezo na  elimu.

Habari kubwa zilizosheheni kwenye kurasa za mbele za magazeti ya leo, karibu msomaji wetu ujisomee.

 

 

 

 

 

 

LIVE MAGAZETI: MAGUFULI AMWAGA MACHOZI KUMLILIA MKAPA, SIMANZI ZATAWALA KUAGWA MKAPA

 

 



source http://www.bongoleo.com/2020/07/31/kinachojiri-kwenye-magazeti-ya-leo-julai-31-2002/