Joyce alifuatwa na kukamatwa baada ya wengi kupiga ripoti kuhusu alivyoanyanganya magari. Picha: Hisani.
Joyce Wairimu Kariuki alikuwa ameiba magari kadhaa kati ya 2018-2019
Alikamatwa Aprili 23, 2019 baada ya kuiba gari aina ya Prado
Si mara ya kwanza Joyce anatumikia kifungo kwa wizi wa mabavu
Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 62 atalazimika kutumikia kifungo cha miaka 35 baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa magari.
Following numerous reports of stolen m/vehicles especially lorries in Nakuru, Nairobi & Mombasa between 2018 and 2019, @DCI_Kenya narrowed down on the suspect around whom the thefts revolved despite having been released from the said prison after completing a 15-year jail term.
— DCI KENYA (@DCI_Kenya) August 4, 2020
Joyce Wairimu Kariuki ambaye pia alikuwa mfungwa katika gereza la Shimo la Tewa alikamatwa Aprili 23, 2019 na kufikishwa mbele ya mahakama Loitoktok alikopatikana na hatia ya wizi wa mabavu.
Kulingana na mkurugenzi wa upelelezi, Joyce alifuatwa na kukamatwa baada ya wengi kupiga ripoti kuhusu alivyoanyanganya magari.
‘’ Kufuaia ripoti kadhaa kuhusu wizi wa magari haswa malori katika eneo la Nakuru, Nairobi na Mombasa kati ya 2018 na 2019, DCI Kenya ilimtafuta na kumkamata mshukiwa huyo licha ya kumaliza kifungo cha miaka 15,’’ alisema DCI.
Joyce alikuwa mwizi wa malori. Picha: Hisani
Baadhi walishangaa na kumuonea huruma bibi huyo ambaye sasa atakumikia jumla ya kifungo cha miaka 60 gerezani wengi wakimshambulia na kutaka apewa adhabu zaidi.
Visa vya wizi wa magari vimepanda vimezidi kupanda, DCI akichukua nafasi ya kuonya wanaohusika kuhusu adhabu kali inayowasubiri.
source http://www.bongoleo.com/2020/08/05/bibi-wa-miaka-62-kutumikia-kifungo-cha-miaka-35-kwa-wizi-wa-mabavu/
No comments:
Post a Comment