Angel Gomes. Picha: Hisani
Angel Gomes Anafunga virago vyake kuondoka Man United baada ya miaka 14
Mchezaji huyo ameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kufeli kufuzu kuwa katika timu ya kwanza
Hatimaye Angel Gomes amefunguka kwa mashabiki wake kuhusu kuihama klabu ya Man United
Mchezaji huyo ambaye amekuwa Man United kwa miaka 14 amechukua hatua hiyo baada ya kukua na kutia makali ujuzi wake bila kufikia nafasi ya kuchezea klabu hiyo kwenye timu ya kwanza.
Angel Gomes joins Lille and is loaned out to Boavista in Portugal for the 2020/21 season.
Wishing @agomes_47 all the best pic.twitter.com/kFTdMvXCzi
— The United Stand (@UnitedStandMUFC) August 4, 2020
Gomes ameamua kuigura klabu hiyo baada ya kukamilisha mkataba wa miaka mitano na kukataa mkataba mwingine licha ya kutakiwa kusalia katika klabu hiyo.
Mchezaji huyo alifunguka kuhusu hatua hiyo huku akiwapongeza pakubwa mashabiki, usimamizi na wachezaji wenza kwa ujumbe mrefu mtandaoni.
‘’ Imenichukua muda maana haikuwa rahisi kuandika hisia zangu. Japo kwa huzuni, wakati umefika kupiga kituo ukurasa mzuri wa maisha yangu kwa miaka 14. Kutoka Salford, Manchester ndiyo yote ambayo nimejua,’’mchezaji huyo aliandika.
‘’Imefika wakati wa kupiga hatua nyingine katika maisha, naamini nyote mtafurahia ninachoazimia. Naitakia klabu na wahusika wote heri, nitawapesa. Pia nataka kuwashukuru mashabiki, ukwasi wenyu haujaenda bila kutambukika,’’ Gomes aliongezea.
Kuondoka kwa Gomes kunajiri wakati ambako wengi waliamini kuwa Ole Gunnar angefanya kila awezalo kuhakikisha kuwa mchezaji huyo anasalia klabuni.
source http://www.bongoleo.com/2020/08/05/nyota-wa-man-united-athibitisha-kuigura-klabu-uhondo-kamili/
No comments:
Post a Comment