Monday, August 3, 2020

Majina matatu yaliyopendekezwa kugombea urais Chadema haya hapa

Mkutano wa Baraza Kuu la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) umepitisha majina matatu ya wanachama waliotia nia ya kuwania urais ambao ni Dk. Mayrose Majinge, Lazaro Nyalandu na Tundu Lissu.

Majina hayo yatapelekwa leo kwenye baraza litapendekeza jina moja litakalopitishwa na mkutano mkuu kesho kwa ajili ya kuwania urais kupitia CHADEMA katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28, mwaka huu.

Aidha, Mwenyekiti cha  Chadema amesema watashirikiana na watu makini na ambao hawatawauza njiani.

“Tunaendelea na mazungumzo na chama kimoja cha ACT-Wazalendo, ” amesema Mbowe



source http://www.bongoleo.com/2020/08/03/majina-matatu-yaliyopendekezwa-kugombea-urais-chadema-haya-hapa/

No comments:

Post a Comment