Monday, January 27, 2020

UNAJIDANGANYA


Eti huwez penda wala kupendwa kisa tu kuna mtu kakuumiza... Mbaya zaid sio Mara yako ya kwanza kuahid hivyo...
Watanzania tupo zaid ya million 50 nusu au robo ni jinsia ya kike kwa kiume. Sasa ktk mailion.ya watu ,mdudu mmoja au 3 hawawez kukufanya uyachukie mahusiano.
" sidhan kama ntakuja mpenda mtu kama nilivyo kuwa nampenda yeye"
Una uhakika na maneno yako?kipi kilicho kufanya uhisi unampenda sana? Unakumbuka ulivyo achana na kumsahau mpenz wako wa 1,sasa huyu wa 5 au 10 ktk orodha yako ana kipi cha maana?
"Siwezi ishi bila penz lake"
Kwan kabla hujafahamiana nae ulikuwa unaishi vipi? Au una ropoka tu ili watu wakuone una uchungu na upendo? Usha kuwa na watu zaid ya 3 toka uyajue mapenz,mbona uliweza wasahau,yeye ana kipi cha ziada?
"Wanaume/wanawake wote ni sawa tu,tamaa ya pesa na ngono."
Una uhakika na maneno yako?
Kwan mpenz wako wa 1,2,3 na 4 wote walikuwa sawa tabia zao? Wote uliachana nao kwa tabia inayo fanana? Wote walikuacha au uliwaacha?
Hatuwez kuwa sawa hata siku moja.. Hasira na chuki zako visikufanye ujiropokee tu.. Au umesahau kuwa Mara kadhaa umekuwa unamsifia rafik yako kuwa mapenz yao yana furaha na Amani?
Hebu subir nawe zamu yako umpate mtu atakae kuonesha utofaut na hao kenge walio tangulia.
Ktk mahusiano
Usijihakikishie sana ukahis hakuna kuachana..mapenz hayana kiapo hivyo badilika kulingana na hali.
Usimlilie sana
Amekufungulia njia kumpata mtu sahihi na bora zaid yake.
Amini kuwa wapo weng walio taman kuwa nawe kipind upo na kunguru wako. Yeye kakuona hufai wapo wanao kuona MPYAAAA
Mtu hodari na makin
Hawez hesabu wanaume au wanawake ulio toka. Badala yake ataendelea pale walipo ishia wengine..Atakutengeza na kesho ukiwa nae utakuwa bora sana mpaka walio kuacha wataman kurud.
Usimlilie mapenz
Lilia uzima ili kesho uonje raha ya upendo wa dhati


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/01/unajidanganya.html

No comments:

Post a Comment