Wednesday, January 29, 2020

Aiiiss aah aah…. Sehemu ya Kwanza (1)πŸ‘‰πŸ‘ŒπŸ’¦

Eddy ameamua kuondoka nyumbani kwa wazazi wake na kwenda kupanga, kwa bahati nzuri anapata chumba katika nyumba moja yenye vyumba sita maeneo ya Mwananyamala kwa Kopa.
Nyumba hiyo imekaa Kiswahili swahili kutokana na wapangaji wanaoishi ndani ya nyumba hiyo.
Kila chumba kimoja kilikuwa na mpangaji mmoja aliyekuwa akiishi na familia yake.
Pia katika nyumba hiyo iliyokuwa na mabanda ya uani, waliishi wapangaji ambao hawakuwa na wake wala waume.
Kati yao walikuwepo wasichana wazuri wenye maumbile ya kupigiwa methali, ambao wengi wao hawakuwa na shughuli maalumu za kuwapatia kipato.
Baba na mama mwenye nyumba nao walikuwa wakiishi ndani ya nyumba hiyohiyo.
Siku ya kwanza Eddy alipokuwa akihamia hakuwa na vitu vingi zaidi ya kitanda kidogo, kabati la nguo na vikombe sita vya chai.
Pia alikuwa na sahani mbili za chakula na jiko moja la Mchina. Kijana huyo aliamua kuanza maisha hayo ya usela japokuwa wazazi wake walikuwa na uwezo mkubwa sana.
Baba na mama yake walimsihi sana kuendelea kukaa nao maeneo ya Kinondoni lakini wala hakutaka kusikiliza ushawishi huo.
Kikubwa alichokuwa akikitaka Eddy ni uhuru, kwani alijiona ameshakua mkubwa, hakutaka kufanya mambo ya uhuni ndani ya nyumba ya wazazi wake.
Mbali na hivyo wazazi wake walikuwa wakimdhibiti sana kijana wao kuingia katika maisha ya kupenda wanawake, hawakutaka ajiingize huko mapema.
Eddy alivumilia ucha Mungu wa wazazi wake kwa kipindi kirefu lakini alipomaliza shule tu hata kabla majibu ya kidato cha nne hayajatoka, akaamua kuhama.
Ushawishi huo aliupata kwa marafiki zake, Salim Raha na John Tupatupa ambao walikuwa na uhuru mkubwa wa kuingiza vyumbani mwao kila aina ya warembo.
Naye alitamani uhuru huo, akaamua kuwaaga wazazi wake na kuondoka katika nyumba ya familia.
Lakini kabla ya kuhama, mara kadhaa kijana huyo alikoswakoswa kunaswa na wazazi wake pale alipoingiza msichana chumbani kwake.
Siku ya kwanza alipoingia katika makazi mapya alikutana na Rehema, msichana wa Kizaramo aliyekuwa ameumbika vyema.
Eddy alishtuka kiasi hata Rehema mwenyewe kuhisi mgeni huyo alikuwa amepagawa kisawasawa. Siku hiyo mrembo huyo alikuwa akisugua miguu yake katika jiwe maalumu lililopo karibu na mlango wa kuingilia msalani.
Rehema alikua ametoka kuoga, akiwa amevaa kanga moja tu iliyokuwa imelowana na maji na kumfanya maungo yake ya ndani yaonekane.
Ndiyo, kanga ilikuwa imeshikana na mwili na kila Rehema alipokuwa akisugua kisigino chake, ndivyo alivyokuwa akimpagawisha Eddy kutokana na kuzalisha mtetemeko wa haja katika mlima aliokuwa ameufungashia nyuma ya mgongo wake.
Kijana huyo alibaki ameduwaa kwa kitambo kirefu akimwangalia Rehema huku akiwa ameshika sahani mikononi mwake lakini Rehema ndiyo kwanza akajifanya kama vile hakuwa amemuona.
Binti huyo akaendelea kufanya kile alichokuwa akikifanya, mara alishtuka aliposikia mlio wa vyombo vikipasuka.
Ndiyo, Eddy alikuwa ameziachia sahani alizokuwa amezishika mikononi mwake bila ya kutarajia.
Kufuatia mlio uliotokana na sahani kuvunjika, Rehema alimgeukia Eddy na kumuuliza kulikoni ndipo kijana huyo alimwambia zilimteleza kwa bahati mbaya.
“Vipi kaka…?” Rehema alimuuliza Eddy.
“Aaah, sahani zimeniteleza kwa bahati mbaya…”
“Pole sana…,” alisema Rehema na kisha kuendelea kusugua visigino vyake huku akitingisha wowowo lake katika staili ile ya hamsini hamsini mia.
“Majangaaa…!” Eddy alisema kwa sauti ya upole na kujilazimisha kuingia ndani ya chumba alichokuwa amepanga.
Kichwani mwake alikuwa akimfikiria Rehema, akawa anajiuliza kama anaweza kuachana na wanawake wote ili awe na huyo.
“Sasa hapa nitamletaje Amina, nitamletaje Anita?” alijiuliza na kuwa na wasiwasi na mwonekano wa Rehema kwa kuwa alikuwa akionekana kama ni mkorofi fulani hivi.
“Anaonekana mshari-mshari sana, sijui kama nitamuweza,” alizidi kufikiria Eddy na kujitupa katika kitanda kilichokuwa kimemaliziwa kufungwa muda mchache na watu waliofika kumsadia.
Ghafla akiwa hapo, alisikia sauti nyingine ya msichana ikimwita Rehema.
“Dada mkubwa… dada mkubwa…”
“Abee,” Rehema aliitikia kwa kuwa ni yeye ndiye aliyekuwa akifahamika kama dada mkubwa ndani ya nyumba hiyo iliyokuwa wakiishi wasichana wengi.
Wengi wao walikuwa wakimheshimu Rehema kutokana na umri wake na uzoefu wake katika masuala ya mapenzi, pia ndiye aliyekuwa mshauri mkuu wa kila jambo kwa mabinti wengine mtaani hapo.
“Njoo uone mambo huku…,” alisema msichana aliyekuwa akimwita Rehema.
“Kuna nini jamani?”
“Patra kafumaniwa huku…,” alisema msemaji huyo na miguu yake kusikika akitoka nje kwa mlango mkubwa wa upande wa barazani.
“Patra…!” alishangaa Rehema na kufanya binti yule kurudia kusema kwa msisitizo.
“Ndiye yeye kwani mtaani kuna Patra wangapi?”
Eddy alikuwa akitaka sana kumuona huyo binti mwingine ambaye alikuwa na sauti nzuri kama kinanda, akili yake ilimtuma kama angemuona angeweza kufanya uchaguzi bora kati ya Rehema na huyo binti.
Ingawaje moyoni Eddy alikuwa amekufa kwa Rehema lakini wasiwasi wake ulikuwa ni jinsi alivyokuwa amekaa kimtoto wa mjinimjini sana.
Hata hivyo hakuweza kutoka kumwangalia msichana aliyekuwa akimwita Rehema, hakutaka kuonekana kama vile ni mmbeya kwa kufuatilia mambo ya watu, akauchuna kwa kuendelea kulala kitandani pake huku akitafakari jinsi atakavyoendesha maisha yake katika makazi hayo mapya.
Mara miguu ya Rehema nayo ikapita katika chumba chake kwa kasi na kutoka nje kupitia mlango wa barazani.
“Daaa huyu mtoto mkali sana lakini…,” alijisemea moyoni Eddy.
****
Siku hiyo Eddy hakutoka nje, kwa kuwa ilikuwa ni jioni hakuona umuhimu wa kufanya hivyo, alikuwa ameshakula na hakujisikia kuoga. Akaamua kuendelea kulala.
Asubuhi siku ya pili, mapema sana Eddy alikuwa ni mtu wa kwanza kutoka nje, akakutana na baba mwenye nyumba na kusalimiana naye.
“Za asubuhi baba?”
“Nzuri tu, umeamkaje?
“Sijambo, shikamoo.”
“Marhaba… tena afadhali umewahi kwenda kuoga ukichelewa hapa… utajuta,” baba mwenye nyumba alisema na kumpongeza Eddy aliyebaki na maswali kibao baada ya kusikia kauli hiyo.
Huku akishindwa kupata jibu, Eddy moja kwa moja akaingia msalani na kumaliza haja zake muhimu na kisha kuelekea bafuni.
Lilikuwa ni bafu la kiswazi ambalo ungeweza kuchungulia na kumuona mtu wa nje kwa kupitia pachipachi za mlango na sehemu za kidirisha kidogo.
Akaanza kujimwagia maji. Hazikuchukua hata dakika tano akasikia milango ikigongana, akaacha kujimwagia maji na kuchungulia nje.
Walikuwa ni wasichana watatu, mmoja alikuwa ni mrefu na mwembamba lakini pamoja na wembemba wake, alikuwa amejengeka vyema katika kiuno kwani alikuwa amekatika na kuwa na kiuno kama cha nyigu.
Mwingine alikuwa ni mnene, mfupi kiasi lakini alikuwa na mvuto wake kutokana na rangi ya mwili wake ambayo ilikuwa iking’aa kwa weusi wake.
Wa tatu alikuwa ni msichana mrefu na mnene ambaye kwa harakaharaka Eddy aliweza kumbaini kuwa ni yule aliyekuwa akimwita Rehema jana yake na kumwambia kwamba Patra kafumaniwa.
Wote watatu walikuwa wakigombania kuingia msalani lakini kwa kuwa yule msichana mrefu na mnene alikuwa na nguvu zaidi yao, akawawahi na kwenda kuingia msalani.
Alipofanikiwa kuingia msalani, wala hakuchelewa kwa kuwa alikuwa amevaa khanga, aliweza kujiachia na kuanza kumwaga haja ndogo kama kuachia bomba la maji huku akisema maneno ya kuwananga wenzake aliokuwa amewashinda.
Kujiachia kwake bomba la maji litiririke bila ya mpangilio, Eddy akajua kuwa huyo binti hakuwa amepata mafunzo ya kutosha.
Eddy alikumbuka siku moja aliwahi kuambiwa na jimama moja kwamba anayekwenda haja ndogo kwa staha ni yule anayejua kujibana na kujiachia taratibu bila ya kusikika sauti kama vile mbwa au ng’ombe.
Hata hivyo, Eddy alikuwa amempenda msichana huyo, ingawaje moyo wake ulikuwa pia umedondokea kwa Rehema. Akawa anasisimka kwa jinsi alivyokuwa akiiachia bomba lake kwa fujo.
“Daaa! Huyu naye sijui ni mtoto wa mwenye nyumba?” alijiuliza.
Hadi alipokuwa akitoka, Eddy aliendelea kumwangalia kupita upenyo, badala ya huyo wakaendelea wasichana wengine waliokuwa wakigombea naye kuingia msalani.
Baada ya hapo, wakafuatia wengine wengi ambao kwa jumla yao wangeweza hata kufikia timu ya mpira wa miguu.
Eddy alishangaa wote hao walikuwa wakiishi vipi katika nyumba hiyo, kama vile haitoshi akajiuliza mbona jana yake wakati alipokuwa akifika, hakuwaona.
“Majangaaa, jamani mbona Majangaaa!,” alisema Eddy kimoyomoyo wakati alipotoka nje na kukutana na wasichana hao kibao wakiwa wamejipanga uwani kwa ajili ya kwenda kuoga.
“Samahani kaka naomba sabuni…” alisema yule msichana wa kwanza aliyewawahi wenzake kwenda msalani akimwambia Eddy.
“Bila wasiwasi,” Eddy alisema na kumkabidhi binti huyo sabuni yake ya kuogea.
“Daa! Unaanza kujipendekeza kwa mgeni,” alisema msichana mwingine na kuwafanya wengine nao waongeze maneno yao kedekede ambayo hata hivyo binti yule hakuyajali.
Baada ya muda binti yule alitoka bafuni na kwenda moja kwa moja kumrudishia Eddy sabuni yake, alipofika usawa wa chumba cha kijana huyo, Irene alikuwa na kusudio moja tu, kutaka kumshawishi ili awe wake hata kabla msichana yeyote anayeishi ndani ya nyumba hiyo hajamnasa.
Alitaka kutumia ushawishi wake kumnasa mwanaume huyo ambaye alikuwa amemvutia kutokana na urefu wake na umbile lake la kimazoezi.
Aliamini kabisa kwamba yeye ndiye aliyekuwa akiendana na mwanaume huyo tofauti na msichana mwingine aliyepanga pamoja na watoto wa baba mwenye nyumba.
Tangu akiwa anamuomba sabuni, msichana huyo alikuwa ameshajua jinsi alivyoutega mtego wake wa kumnasa kijana huyo.
Alitoka msalani akiwa amevaa kanga moja iliyokuwa ameilowanisha maji na kujaribu kujitingisha kwa mwendo wake wa madaha, moja kwa moja akawapita wasichana wengine waliokuwa wakigombea nafasi ya kwenda kuoga baada ya yeye kutoka.
Alitembea kwa mwendo huo uliojaa uchokozi na kisha kuusogelea mlango wa chumba cha Eddy, bila ya kubisha hodi akaufungua kidogo na kuchungulia, wakati huo macho yake alikuwa ameyaachia kwa kuyalegeza na kuyafanya kama yatake kudondoka.
“Kaka samahani sabuni yako hii…” alisema akiwa ameuingiza uso wake ndani ya chumba cha Eddy aliyekuwa akivaa kwa ajili ya kujiandaa kutoka.
Eddy alishtuka na kumfanya binti huyo naye kujidai kumuomba radhi kwa kitendo alichokuwa amekifanya lakini wakati akifanya hivyo, tayari mwili wake wote ulishakuwa ndani ya chumba cha kijana huyo.
“Naitwa Irene…” alisema huku akionekana kukikagua chumba kile kama vile alikuwa ametumwa kwa ajili ya kufanya kazi ya ukaguzi.
Eddy alikohoa kidogo kutoa kikohozi kikavu kisha akamjibu:
“Miye naitwa Eddy au Eddyson Manyara,” wakati huo kijana huyo alikuwa akichomekea shati lake.
“Oooh oooh jina zuri sana… naona ndiyo unaanza maisha?” alisema Irene akiwa anamwangalia Eddy baada ya kukagua chumba hicho na kukiona kila kilichokuwemo ndani yake.
“Eeehe, nimeamua kuondoka kwa wazazi na kuishi peke yangu ili kujipanga zaidi,” Eddy alisema kwa aibu.
“Kwa hiyo umekuja kwa walimu tukufunze maisha?”
“Sijakuelewa…?” alihoji Eddy.
“ Siku zote Waswahili husema anayeshindwa na wazazi hufunzwa na walimwengu, siye ndiyo walimwengu wenyewe… karibu sana na jisikie kama uko nyumbani kwa wazazi wako.”
“Aaah aaah…” Eddy alicheka na kuendelea kuvaa shati lake tayari kwa kutoka nje ya chumba chake na kwenda kwenye mihangaiko yake.
“Unafanya kazi?” Irene alimuuliza Eddy.
“Yaa, nafanya kazi…”
“Sawasawa karibu sana…” alisema Irene huku akifungua mlango na kutoka nje kwa madaha, akijitahidi kuutingisha mwili wake.
Wakati Irene akitoa mguu wake nje ya chumba hicho ghafla alipoinua uso wake kuangalia mbele akakutana uso kwa uso na Rehema akiwa anapita kwa ajili ya kwenda uwani.
Rehema hakuonekana kumchangamkia Irene ambaye ndiyo kwanza walikuwa wakionana tangu kulipopambazuka siku hiyo.
“Za asubuhi dada?” alisema Irene kumwamkia Rehema kwa haraka huku akichekacheka lakini salamu yake haikuitikiwa, akabaki ameduwaa.
Rehema alimpiga jicho kali Irene kwa kumshusha na kumpandisha kisha akaenda zake uwani hali iliyomfanya Irene kufadhaika, moja kwa moja akajua kuwa ameingia kwenye vita na malkia wa nyumba hiyo.
Irene alijaribu kufikiria ni nini kimetokea kati yake na Rehema lakini hakuambua kitu. Alifikiria labda jana yake alikuwa amemkosea, pia hakukumbuka kutokea kitu kama hicho.
“Hivi huyu brother men anaweza kuwa chanzo?” alijiuliza akimfikiria Eddy.
Irene akiwa katika mawazo hayo akasema kama kweli chanzo ni huyo kijana, basi atahakikisha kwamba anakula naye sahani moja ili kuzidi kumvimbisha mashavu Rehema.
“Malkia malkia… wala sitajali kama ni malkia wa nini, watu tumewaona mamalkia wa maana atakuwa yeye malkia wa vichochoroni,” alisema Irene na kisha akaachia msonyo wa nguvu uliosikika hadi nyumba ya pili.
Wakati huo alikuwa ameshaingia chumbani kwake na kuanza kujikwatua kwa kuupara uso wake kwa mapambo ya kila aina ambayo yalipaswa kuingia usoni pake.
Wakati akiendelea kujipamba kila dakika ilivyokatika ndivyo alivyokuwa akikikumbuka kitendo alichofanyiwa na Rehema.
Alikasirika sana kuona anamsalimia halafu anamvimbishia mashavu bila ya kujua sababu, kila alivyokumbuka kitendo hicho aliachia msonyo na kuendelea na shughuli zake.
“Asubuhi asubuhi mtu anakuharibia siku,” alijisemea peke yake Irene wakati akijiangalia kwenye kioo kisha akaachia msonyo mwingine.
****
Kwa upande wake, Rehema roho yake ilikuwa imemchafuka, ikimchonyota kwa kumuona Irene akitoka chumbani kwa Eddy, moja kwa moja akajua kuwa wawili hao watakuwa wamelimenya tunda la mwituni asubuhiasubuhi.
“Haiwezekani lazima watakuwa wamepeana kile kitu roho inapenda, iweje atoke chumbani kwake asubuhi yote hii?” alijihoji na kukosa jibu la uhakika.
Rehema alikuwa amechukia kwelikweli na moyo wake ulimuuma kwa kuona kwamba Irene anaanza kuwa na uhusiano na mwanamme huyo mgeni kabla yake.
“Atakuwa ameingia asubuhi ileile au atakuwa amelala chumbani kwake?” alijiuliza tena Rehema huku donge likiwa limemnasa rohoni mwake.
“Yaani atakuwa ameshanizidi kete?” aliwaza Rehema ambaye aliamini kabisa kwamba mitego aliyomtega Eddy siku ya kwanza ilikuwa ni lazima amnase kwanza kabla ya kinyangaratika kingine ndani ya nyumba yao.
****
Kwa upande wake Eddy ambaye alitoka baada ya kujipulizia utuli uliouteka ukumbi wa nyumba hiyo, alikwenda moja kwa moja kwenye shughuli zake kubaingiza, kwa kuwa bado hakuwa na kazi ya kufanya.
Alikuwa akifanya kazi yoyote ambayo aliamini kuwa ingeweza kumwingizia kipato.
Siku hiyo alikwenda moja kwa moja hadi kijiweni kwake maeneo ya Kariakoo ambako vijana wengi hukutana na kuuza maneno kwa watu wengine ili wapate chochote kitu.
Moyoni mwake Eddy hakuwa salama hata kidogo, kwa kuwa vitendo viwili vilikuwa vikimchanganya akili yake kwani moyo wake ulikuwa ukiripuka kila alipokuwa akikumbuka jinsi alivyomuona Rehema akisugua kisigino chake ilhali amevaa khanga moja iliyokuwa imelowana sehemu za makalioni.
Moyo ukitulia unaripuka tena kwa kitendo cha Irene kuingia chumbani kwake akiwa na khanga moja ambayo nayo ikiwa imelowana, Eddy alivuta taswira za mabinti hao wawili na kubaki akiwa hana la kufanya.
“Kila mmoja ana uzuri wake…” Eddy aliambia nafsi yake na kubaki na dukuduku moyoni mwake. Mpaka wakati huo hakuwa akijua kama amesababisha songombingo kati ya wasichana wawili hao.
Hilo hakulijua kwa kuwa hakuliona wakati likitokea, kwa sababu alikuwa chumbani kwake, laiti kama angeliona angejua cha kufanya, asingekuwa na budi kuchagua upande mmoja.
Lakini moyo wa Eddy ni kama wa wanaume wengine, haukulidhika na mmoja, unataka kumi na moja kwa kutaka kuonja kila sehemu ili kujua radha yake.
Eddy alikuwa akitaka kujua utamu wa Rehema lakini pia alikuwa akitaka kujua utamu wa Irene kwa kuwa damu yake ilikuwa ikichemka, kikubwa alikuwa akijiuliza itawezekanaje ndani ya nyumba moja!
Hilo ndilo lililokuwa likimitia mashaka, vinginevyo alikuwa akiwataka mpaka wengine waliokuwa wakiishi ndani ya nyumba ile kwani aliamini kuwa kila mti una tunda lake na kila tunda lina utamu wake.
Eddy alikwenda mjini na kuzugazuga kwa jamaa zake maeneo ya Shule ya Uhuru Karikooo, huko alikutana na marafiki zake Spider au Raha na John Tupatupa na kuongea nao kile kilichomkuta katika nyumba ile aliyohamia.
“Hapo lazima ucheze kama Pele lakini kwa jinsi unavyonihadithia kitu hapo ni Rehema…” alisema Raha.
“Mmmh mwana usipepese macho wala kuuma meno, hapo kitu ni Irene…” aliongeza John Tupatupa ambaye alimlaumu Eddy kwa nini hakumaliza mchezo wakati mzigo ulipoingia chumbani.
“Washikaji sasa mnanichanganya… niacheni nitumie akili yangu,” Eddy aliwaambia baada ya kuona kila mmoja akiwa na mtazamo wake kuhusiana na mabinti hao.
****
Rehema hakuwa ameridhika, alipofika uwani alipishwa kwenda msalani na mabinti waliokuwa katika foleni kwa kuwa yeye ni malkia wa nyumba hiyo.
Akaoga na kumaliza haja zake muhimu, kama kawaida alipotoka alisugua miguu yake huku akiwa na hamu ya kutaka kujua Irene aliingiaje chumbani kwa Eddy.
Alipomaliza shughuli zake akamchukua mmoja wa mabinti waliokuwa wakisubiri kwenda kuoga na kumwambia amfuate chumbani kwake.
Binti akajua labda ametafutiwa mtu wa kuduu naye, akawa na wasiwasi wakati alipokuwa akiambiwa kuingia chumbani kwa malkia.
“Usiogope kaa hapo kwenye sofa…” alisema na binti akiwa na wasiwasi akaketi.
“Ulimuona Irene leo?”
“Ndi… ndi- yoooo, nilimuona dada…”
“Ulimuona wakati gani?”
“Alipokuwa akitoka kuoga…”
“Hukumuona alipoingia chumbani kwa yule mgeni…?”
“Wala sikumuona lakini kama aliingia atakuwa alikwenda kumrudishia sabuni yake…”
“Kwani alichukua sabuni kwake?”
“Eeeh wakati akiwa anatoka kuoga yule mkaka, dada Irene akamuomba sabuni ya kuogea…” alisema binti yule na kuifanya roho ya Rehema kuanza kupona kidonda cha wivu kilichokuwa kikimkereketa.
“Oke nenda, usimwambie yeyote nilichokuuliza.”
“Sawa.”
Baada ya binti yule kutoka nje, Rehema alifurahi sana, akajua kuwa Irene hakuwa ameambulia kitu. Akafurahi na kujitupa kitandani na kukumbatia mito.
Baada ya muda kidogo Kijana Eddy alirudi kutoka kwenye mihangaiko yake
koridoni alikutana na Baba mwenye nyumba na kuanza kusalimiana,,,,,wakati wanaendelea kuongea umbe rehema alisikia na kutoka nje wakati huo Baba mwenye nyumba alikuwa ameshaingia chumbani kwake
“rehema alipomuona eddy akaaanza kutembea kwa madoido
Kisha akajitingisha mwili wake kuonesha kwamba alikuwa mpana na kuifanya khanga aliyoivaa kutikisika kutokana na mtikisiko uliosababishwa na ‘boksi’ lake lililokuwa limetanuka kisawasawa nyuma ya mgongo wake.
Wakati Eddy alipokuwa akikaribia kumfikia akajikohoza ili kuweka sauti yake katika ile hali aliyokuwa akiitaka yeye.
Alikuwa amedhamiria kutoa sauti ile yenye mvuto ambayo ingeweza hata kumtoa nyoka pangoni.
“Mambo?”
“Powa,” alijibu Eddy akiwa ameshtushwa sambamba na kupigwa na mshangao kutokana na bashasha alizokuwa ameoneshwa na Rehema.
“Pole na mihangaiko…” Rehema alimwambia tena Eddy aliyekuwa bado akili yake haijakaa sawasawa kujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea.
“Asa… Asante,” alijibu bila ya kujiamini.
Muda wote huo Rehema alikuwa akiitumia siraha yake ya macho, pamoja na kwamba giza lilikuwa limeshaanza kuingia lakini machao yake makubwa na meupe ‘pee’ yalikuwa yaking’aa kama nyota ang’avu.
Ghafla, Rehema akalipokea gazeti lililokuwa limeshikwa na Eddy, wakati kijana huyo akiendelea kushangazwa na ukarimu huo, alijikuta akishikwa mkono na kukaribishwa ndani.
Baada ya kufika ukumbini, moja kwa moja Rehema ambaye alikuwa ametangulia mbele, akabadilisha mwendo, akawa anatembea kwa kulitingisha boksi lake kama vile alikuwa akitaka kuliangusha.
Mbaya zaidi kuna wakati alikuwa akisimama ghafla na kumgusa Eddy kwa makalio yake na kumchanganya.
Eddy alikuwa kama nyoka wa kibisa hakuwa na sumu kabisaaa, makali yake yote yalikuwa yamekwisha na ujanja wake ulikuwa umetiwa mfukoni kwani kama ni shambulio basi lilikuwa la ghafla sana kumkumba, hivyo hakulitegemea.
Hakuweza kujihami kwa njia yoyote ile, alibaki akipelekwa kama gari bovu lililokuwa limekatika breki.
Bila ya kutarajia akajikuta akiingizwa chumbani kwa Rehema badala ya kuelekea chumbani kwake.
“Karibu…” alisema Rehema kwa sauti laini ya kuweza kumpagawisha mwanaume yeyote rijali.
Eddy hakuamini kile alichokiona chumbani humo, kilikuwa chumba kikubwa kilichokuwa katika mwanga hafifu wa rangi nyekundu na kumfanya ashindwe kukiona kila kitu katika uhalisia wake.
Alijaribu kuzungusha macho yake ndani ya chumba hicho kila pembe, alipomaliza akaanza kumwangalia mwanamke huyo ingawaje kwa kumwibia.
Eddy mbele yake kila kitu kilikuwa kizuri, alivutiwa na kila kitu, alivutiwa na macho ya Rehema yaliyokuwa yaking’aa, alivutiwa na rangi ya mwanamke huyo, akavutiwa na umbile lake.
Eddy alishangazwa na uzuri wa Rehema ambaye kwa wakati huo aliuona uzuri wake ulikuwa umezidi maradufu ya siku alipomuona kwa mara ya kwanza mchana.
“Karibu sana….” sauti laini iliyakatisha mawazo ya Eddy na kuyafanya arejee chumbani humo.
Pamoja na usiku huo kutaliwa na kibaridi cha haja lakini kijasho chembamba kilianza kumtoka nyuma ya mgongo wake kutokana na uti wa mgongo wake kupatwa na mshtuko.
“Utakunywa nini…?” Wakati Rehema akiuliza swali hilo tayari alikuwa ameshafika kwenye kochi alilokuwa amekaa Eddy na kuinama kwa heshima akiwa amepiga magoti akimwangalia kwa macho yake makali ambayo yalikuwa na uwezo wa kuyaona hata mapigo ya moyo ya mwanaume huyo yalivyokuwa yakienda kwa kasi.
“Nitakunywa chochote…” alisema Eddy akiwa amejiinua kidogo katika kochi na kisha kujirudisha tena chini.
“Usijali, nitakupa juisi ya ndimu…” alisema Rehema na kusimama kisha akainuka na kukifuata kijokofu kidogo kilichokuwa katika kona ya chumba hicho.
Pamoja na utoto wake wa mjini, Eddy hakujua kama duniani kulikuwa na juisi ya ndimu, hakuamini alipoambiwa kwamba analetewa juisi hiyo.
Kama kawa Rehema hakuacha kulitingisha boski lake pale alipokuwa akimpa mgongo kijana huyo na kufuata kile alichokuwa akikifuata, hali iliyokuwa ikimweka katika wakati mgumu sana Eddy.
***
Awali ‘paka’ wa Eddy alikuwa akishindwa ‘kulia nyau’ lakini kadiri muda ulivyokuwa ukisonga mbele ndivyo alivyoyazoea mazingira na paka wake akaanza kututumka na kuvimba huku akilia nyau baada ya kuona kwamba kulikuwa na kila dalili za kula ‘samaki’.
Rehema alirudi na juisi iliyokuwa ndani ya glasi, ambayo hakutaka kuiweka juu ya stuli wala hakutaka kuiweka juu ya meza iliyokuwa hatua chache kutoka alipokuwa amekaa Eddy.
Akakaa katika kochi sehemu ya kuwekea mikono na kuishika vyema glasi hiyo na kuipeleka kinywani kwa kijana huyo.
Eddy hakuwa na ujanja, akaachia mhemo wa nguvu na kisha akatanua kinywa chake na kuipokea juisi hiyo na akanywa funda moja.
Hakutegemea utamu wa juisi hiyo, akiwa anatafakari akapewa tena, naye hakijivunga akapiga funda lingine, hakutarajia kuipata radha aliyoipata, ilikuwa ni juisi nzuri iliyochangamsha mdomo na mwili wake kwa jumla.
Hali iliendelea hivyo mpaka juisi ilipoisha, mpaka hapo akawa ameshaelewa kwamba alikuwa ametekwa kimapenzi na Rehema.
Akajiuliza maswali mengi, hakuamini kama alistahili kufanyiwa yote aliyokuwa akifanyiwa lakini hakuwa na budi kukubali kila alichokuwa akifanyiwa na binti huyo mwenye umbile matata.
“Unaitwa nani vile…?” Rehema alijifanya hamjui vyema Eddy.
“Eddy… Eddy Manyara… mtoto wa pili kwa mzee Manyara…” kijana huyo alijikuta akishusha historia yake kwa ufupi. Kutokana na hali aliyokuwa nayo angeweza kusema kila kitu alichokifanya alikuwa amepagwa na mambo machache aliyokuwa amefanyiwa kwa muda mchache.
Eddy akaamini yale yote aliyokuwa akiyasikia mitaani kwamba wanawake wa Kitanga ni noma katika mahaba, akajua amepatikana ingawaje hakuwa akijua Rehema ni kabila gani.
***
Wakati yote hayo yakitendeka Irene alikuwa amelala chumbani mwake fikra zake zikipanga mikakati ya kumnasa Eddy ili kumdhihirishia Rehema kwamba yeye ni kiboko yake .
Akiwa amejilaza kitandani, ghafla mlango wake ulifunguliwa, akaingia mdogo wake aitwaye Patricia akionekana kama kuwa na ujumbe mahususi kwa ajili yake.
“Vipi?”
“Dada nimekuja…”
“Kwa heri au kwa shari…”
“Kwa kweli sijui kama ni kwa heri au kwa shari.”
“Kwa nini?”
“Nataka nikwambie kitu cha ajabu nilichokiona…”
“Kitu gani?”
“Ni kuhusu dada Rehema na yule mgeni wa chumba…” Patricia aliposema hivyo tu, kwa kasi ya ajabu Irene aliinuka kutoka katika kitanda na kujikuta amekaa katika tendegu la kitanda.
“Wamefanya nini?”
“Tulia nikupe habari…” alisema Patricia baada ya kugundua dada yake ameshtushwa na kauli yake kuhusu Eddy na Rehema.
“Wamefanya nini?”
Patricia akaanza kumpa mkanda mzima, kwanza alianza kumwambia eneo alilokuwa amekaa.
“Nilikuwa nimekaa nyumba ya jirani pamoja na akina Edna, Jack na Amina…” alianza kuhadithia Patricia.
Kisha Patricia akamwambia dada yake jinsi Eddy alivyopokelewa na Rehema kisha akamwambia kwamba na wenzake wakaamua kuufuatilia mchezo mzima ulivyokuwa ukiendelea.
Kama vile haitoshi akasema wenzake walivyoshindwa kuendelea, yeye alifuatilia na kushuhudia vituko vyote alivyokuwa akifanyiwa Eddy na Rehema hadi akashuhudia wawili hao walipokuwa wakiingia katika chumba cha Rehema.
Hivyo, akatumia fursa hiyo kumwabarisha dada yake kila kitu alichokishuhudia.
“Unasema kweli?”
“Kweli dada…”
“Haiwezekani…” alisema Irene na kuinuka, akachukua khanga yake na kujifunga kiunoni na kutoka chumbani humo kama mshale huku Patricia au Pat akimfuata kwa nyuma.
“Unaenda wapi dada?” Pat alimuuliza.
“Nifuate huku…” alisema Irene huku akielekea upande wa uwani, kitu ambacho kilimshangaza Pat kwa kuwa alijua dada yake angeweza kwenda kugonga mlango wa Rehema na kumuulizia kama Eddy alikuwa chumbani humo.
Moja kwa moja Irene alitokea uwani, Pat hakuwa na budi kumfuata, Irene alipofika uwani akakata kulia na baada ya mwendo mbele kidogo akakata tena kulia, akawa analifuata dirisha la Rehema.
Hapo ndipo Pat alipofunguka kimawazo kwa kujua kuwa dada yake alikuwa akienda kuchungulia dirishani ili kuthibitisha kama kweli yule mgeni alikuwa mle chumbani.
Baada ya kuhisi hivyo, Pat alipunguza mwendo kwa kuamini kuwa dada yake atashuhudia mwenyewe kile alichomwambia, alihisi dada yake hakuwa akiamini maneno ya kuambiwa bali alikuwa akitaka kushuhudia mwenyewe.
Wakati Pat akiwaza hivyo, Irene alishachukua kijiti kilichokuwa pembeni na kuanza kupekenyua dirisha la Rehema kwa kulisogeza pazia pembeni, akaruhusu mboni zake zipenye na kuchungulia ndani.
“Ah!” aliachia mshtuko mdogo baada ya kushuhudia kile kilichokuwa kikiendelea ndani. Aliwaona kwa macho yake Rehema na Eddy wakiwa katika mazingira tata.
Eddy alikuwa amekaa kwenye kochi, Rehema alikuwa ameinama mbele yake akiwa amepiga magoti, hilo halikumshtua Irene bali alishangazwa na kitendo kile kilichokuwa kikiendelea kati ya wawili hao.
Mbali na Rehema kupiga magoti mbele ya Eddy lakini kitendo kilichokuwa kikiendelea ndicho kilichomshtua na kumfanya mapigo yake ya moyo yaongeze kasi, Rehema hakuwa ameinama bure bali alikuwa akiumenya ‘mua’ wa Eddy kwa mdomo.
Irene akaganda pale dirishani akitumbua macho kama mjusi aliyebanwa na mlango huku akimshuhudia mwenzake alivyokuwa akionesha ufundi wa kuumenya mua kwa mdomo.
Akiwa dirishani, mate yakamjaa mdomoni akayameza funda moja kama mtu aliyekuwa akitafuta kitu cha kufanya lakini hakuweza kufanya chochote, ndani ya nafsi yake akakiri kwamba anatakiwa kujipanga vyema ili kushindana na Rehema.
Alikiri uwezo wa mwanamke mwenzake huyo ulikuwa mkubwa katika kumpagawisha mwanaume baada ya kushuhudia tukio lile, wakati Irene akiendelea kuchungulia, Pat naye akapiga hatua kumfuata pale dirishani.
Irene alihamisha macho na kumwangalia kisha akamuonya kwa ishara ya kuweka kidole cha shahada mdomoni mwake akimtaka kuchukua tahadhari kutokana na hatua zake ili asipige kelele.
IRENE aliporudisha macho kuangalia chumbani akakuta zoezi limebadilika, safari hii ilikuwa ni zamu ya Eddy kufanya kitendo kile alichokuwa akikifanya Irene.
Kijana huyo alikuwa amempisha Rehema kwenye kochi na msichana huyo akaulaza mgongo wake kwenye kochi hilo na kuachia vimbwanga vyake vyote hadharani.
Eddy alikuwa amepiga magoti mbele yake na kufanya kama alivyokuwa akifanya Rehema, alikuwa anakula kitu roho inapenda, ulimi wake ulikuwa ukifanya kazi ya kupita na kusafisha kila pembe ya kile kitu ambacho kilimfanya Rehema apewe jina la Rehema na katu si jina la jinsi nyingine.
Ulimi wa Eddy ulikuwa kama una ufagio wenye msasa ambao ulikuwa ukipita kila kona na kusafisha uchafu wa aina zote.
Hali hiyo ilimfanya Rehema kuanza kulalamika kwa kupiga kelele ambazo zilimfanya Irene kusisimka na kutaka kujua hisia za Rehema.
Alitamani katika nafasi ile angekuwa yeye ili aweze kuona kile kilichokuwa kikimfanya alalamike kwa kupiga kelele.
Mbali na Irene, kelele zile pia zilimsisimua Pat ambaye kwa wakati huo alikuwa akishuhudia vitu adimu katika maisha yake.
Kitendo hicho hakikuwa kipya kwa Irene ambaye alikuwa ameshawahi kukisikia kwa watu ingawaje hakuwahi kuona kikifanyika.
Msichana huyo alishawahi kusikia baadhi ya wasichana wenzake wakizungumzia jambo hilo. Siku moja akiwa na wasichana hao walikuwa wakipiga stori zao za chumbani.
Kila msichana alikuwa akieleza uzoefu wake jinsi alivyokutana na mwenza wake na kumfikisha pale kwenye kilele cha mlima mrefu kuliko yote Afrika kama siyo duniani.
Hapo, ndipo Irene aliposikia kwamba kuna kitu kama hicho ambacho kila mmoja alikiita kwa jina lake, mmoja wa marafiki zake alikibatiza kwa jina la ‘special menu’.
“Yaani ukiliwa special menu unaweza kupagawa na kuwa mwendawazimu…” alisema rafiki huyo kumwambia Irene ambaye hakuwa akielewa vyema maana ya kitu hicho.
Hata alipoeleweshwa hakuamini kama kilikuwa kikiwezekana kwa kuwa ilikuwa ni vigumu kwake kuweza kumwachia mtu wa jinsi nyingine aingie kwenye himaya yake na kufanya kitu kama kile.
Siyo kitendo hicho tu, Irene wa kipindi hicho alikuwa hawezi hata kumwachia mwanaume aiangalie ikulu yake, nini kuila kama peremende.
Hivyo siku hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kuona special menu ikiliwa.
Kwa upande wake Pat, hakuwa amesikia popote kama kulikuwa na kitu kama hicho, alikuwa mchanga sana katika fani ya mahaba. Ndiyo kwanza alikuwa akipevuka na kutaka kuingia katika dunia hiyo.
Mbali na kutojua kitu hicho kwa siku hiyo, alikuwa akishuhudia kwa mara ya kwanza kwa macho yake. Pat alishangaa sana na kujiuliza maswali mengi ambayo kichwa chake kilishindwa kuyajibu.
“Anamuuma?” alijiuliza.
“Anamla…?” lilikuwa swali lingine tena ambalo nalo halikupata jibu.
***
Ghafla mchezo ulibadilika tena na kuingia kwenye hatua nyingine, hali hiyo iliwapa wakati mgumu sana Irene na mdogo wake Pat.
Kwanza Irene alishangazwa na ‘chachandu’ za Rehema ambazo zilikuwa zimefunika sehemu kubwa ya mwili wake.
Yeye hakuwa nayo hata moja, hapohapo aliapa kwamba lazima kabla jua la kesho yake halizajama aende Kariakoo na kutafuta zake.
Hakutaka mjadala katika hilo, aliamini kuwa amejifunza kitu na kwa kuwa alishaamua kuingia katika vita na Rehema, basi hakuwa na budi kujipanga ili kumkabili adui kwa nguvu zote.
Roho ilimuuma sana Irene, alitamani kulisimamisha pambano hilo lakini hakuwa na uwezo huo, ilimbidi kuangalia pambano hilo huku roho ikimuuma.
Rehema na Eddy wakaingia kwenye hatua nyingine ya kusaula viwalo vyao katika maungo na kuingia uwanjani kusakata kabumbu, hata hivyo uwanja uliotumika haukuwa ule wa kawaida.
Rehema na Eddy walikuwa wameamua kupiga shoo kwenye uwanja wa chandimu, hawakutaka kuingia kwenye dimba kubwa, waliamua kucheza gemu hilo kwenye uwanja mdogo wa fundi seremala yaani kwenye kochi huku wakiliacha dimba kubwa katika hali ya usalama.
Rehema na Eddy ni kama vile walikuwa wamepaniana, kila mmoja kama alikuwa akitaka kumuonesha mwenzake ufundi wa jinsi anavyojua kusakata kabumbu.
Nini kiliendelea? KUSOMA sehemu Inayo Fuata 
||
V


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/01/aiiiss-aah-aah-sehemu-ya-kwanza-1.html

No comments:

Post a Comment