Tuesday, January 28, 2020

KABLA HUJAINGIA KATIKA TAASISI YA NDOA ANGLIA HAYA



No photo description available.
1. Itazame hasira yako. Jifunze namna ya kuidhibiti. Hasira hubomoa ndoa.

2. Angalia sana suala la mapenzi holela. Zinaa hubomoa ndoa. Usifanye khiyana dhidi ya mwenza wako.

3. Angalia kiwango cha ukomavu wako. Ndoa inahitaji ukomavu, khasa wa kiroho.

4. Angalia uchumi wako. Unahitaji kipato halali kwa ajili ya mahitaji halali ya familia yako.

5. Angalia sana uaminifu kati yako na mwenza wako. Muamini mwenza wako. Usifunge ndoa na mtu usiyemuamini.


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/01/kabla-hujaingia-katika-taasisi-ya-ndoa.html

No comments:

Post a Comment