Tuesday, January 28, 2020

SIFA KUU YA MWANAMME MAKINI


Image may contain: 2 people, people smiling
Mwanaume makini ni yule ajuaye makosa yake amtendeayo mkewe!

Kukosea ni ubin adam maana hakuna aliye mkamilifu, Lakini Basi ukimliza ujue na kumnyamazisha... ikiwa utamliza halafu umuache anyamaze mwenyewe nakuambia NI HATARI KULIKO UBAYA ULOMTENDEA!

Bin adam yeyote anao moyo wa nyama na anajuwa kuumia sasa usiruhusu kiburi kikakupanda ukamuumiza mtu halafu ukachukulia poa kisa machozi ni maji tu akinywa yatajaa Mengine.

Rafiki muogope Mwanamke ambaye analia na kunyamaza mwenyewe, Mwanamke huyo usifikiri akinyamaza mwenyewe Basi wewe ni mshindi laa hasha!

Moyo wa Mwanamke huyo unajaa maudhi na mwisho wake ni mbaya, Mrejeshe mkeo katika hali ya furaha kila mnapotofautiana kwa kufanya hivyo UTASAMEHEWA KWELI ila kama utamliza na akanyamaza mwenyewe halafu useme NISAMEHE MKE WANGU Basi anaweza kusema NIMEKUSAMEHE lakini isiwe kweli.

Jifunze kumbembeleza mkeo kila uonapo umemkosea na hilo ndilo liletalo maana ya UPENDO lakini ukimkosea halafu ukajifanya kidume sana SIKU UKIKUTANA NA HASIRA YAKE usimtafute Shetani Kwani wewe ndiye Chanzo cha hayo


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/01/sifa-kuu-ya-mwanamme-makini.html

No comments:

Post a Comment