Saturday, February 29, 2020

YAJUE MAMBO YANAYOUA MAHUSIANO NA NDOA NYINGI!


Image may contain: 2 people, people standing, shoes and outdoor
NDUGU.
JAMII.
MTOTO/WATOTO.
MARAFIKI.
WIVU WA KI MAENDELEO.
SIRI.
UBINAFSI.

Hawa ndiyo maadui nambari moja kwenye MAPENZI na kama unashiriki nao ni ngumu kuwa na mahusiano IMARA
Ndugu anabaki kuwa ndugu, Kwa vyovyote vile MAPENZI ni jambo binafsi otherwise wewe ndiye usababishe ndugu kuingilia Mahusiano/ndoa yako kitu ambacho ni hatari, NDUGU hajui radha na yote uyapatayo kwa mwenza wako sana sana anaweza kuwaka wivu akakuharibia kwa dhamana ya UNDUGU.
Jamii haiwezi kuwa sehemu ya FURAHA NA AMANI yako hivyo ni jikumu lako kuweka mipaka juu ya mtu kutaka kujua yaliyopo kwenye UHUSIANO/NDOA yako vinginevyo unaweza kusababishiwa aibu hata usiweze kutembea na mwenza wako kwa kuhisi WANAKUCHEKA.
Mahusiano/ndoa nyingi za sasa unakuta mtu tayari ana mtoto/watoto ambao alizaa na mtu mwingine kwa namna yoyote ile unaweza kujikuta unaona kama unamuonea/unawaonea watoto wako kwa kudhani uhusiano/ndoa uliyopo nje ya mzazi wao kwao ni ki kwazo kumbe ni ile hali ya ubin adam inayowapata watoto kwa kudhania Baba au Mama mpya hawezi kuwapenda kitu hicho kitawafanya kutompa UPENDO Mtu uliyenae, Mwisho kabisa utahisi Mtoto/watoto wako hawaupendi UHUSIANO/NDOA uliyopo, Na hapo taratibu PENZI LITAZAMA.
Marafiki hawa bwana ujue kila mmoja na mtazamo wake, Unaweza kupata Mtu wao wasimpende ama wakasikia wivu kwa namna unavyopendwa sasa usipokuwa makini wewe mwenyewe utajikuta huna msimamo mwisho kabisa kuhisi marafiki wanakuwazia mema mara moja utamuacha Mtu wako bila sababu.
Wivu wa kimaendeleo hapa napo panayo changamoto, Unajua Kuna watu hawapendi uwe na kitu kizuri kama hajakufanyia yeye na mara nyingi watu hawa ni wale WANAOPENDA Mtu asiendelee kwa kuhofia kumkosa Mwenza wake, Ni rahisi kuharibu uhusiano/ndoa ikiwa mwenzio atabaini hupendi maendeleo yake.
Siri ni nzuri lakini ujue kutofautisha yahusuyo siri, Kama unafanya uzinzi wewe ficha tu japo iko siku ufichayo yatakuwa wazi, Lakini kama unaficha mpaka mambo ambayo kwa uhalisia mwenza wako ni haki yake kuyajua Basi tambuwa kwamba kwa kuyabaini kwake bila wewe kusema NI NJIA RAHISI KWAKE KUANZA MASHAKA JUU YAKO na mara nyingi ukuta wa maelewano UTAJENGWA na mwisho kabisa ni migogoro isokwisha.
Ubinafsi ni SHETANI NAMBA MOJA KWENYE MAHUSIANO/NDOA YEYOTE hata kama uonyeshe upendo mkubwa namna gani mwenza wako akijuwa wewe ni mbinafsi ni rahisi kukutungia sheria kitu ambacho kitaleta vita ya ki MAENDELEO kwamba kwa sababu wewe vyako Mimi sipati Basi na vya kwangu sikupi, Mwisho kabisa ni kelele zisizo na mashiko.
Maana ya Mahusiano/ndoa na MAPENZI kwa ujumla wake ni mmoja kuunganisha nguvu zake na za mwingine na kujenga THAMANA YA KUWA WAMOJA kwa namna yoyote Wawili hao wanawajibika kila mmoja KUJUWA THAMANI YA MWENZA WAKE NA KUMTHAMINI hapo utakomboa uhusiano/ndoa yako kwa urahisi kabisa, Fikiria zaidi kuwa WAZI kwa Mwenza wako itakufanya hayo yote ambayo ndiyo chanzo cha mmomonyoko wa PENZI LAKO kutokuwepo💪
Unapoingia kwenye MAHUSIANO/NDOA hayo mambo yakemee na Uweke ukuta yasiingie kwako ili ulifanye Penzi lako kuwa IMARA na hapo Mito ya FURAHA NA AMANI itakufuata💃💃
Sasa ujifanye RUTHU ushakuwa na Mahusiano/Ndoa halafu kutwa kugeuka nyuma kuwatazama ndugu, jamii, marafiki, wanasema nini ITAKULA KWAKO😅
Mwisho wao kabisa mchana lakini ukienda KULALA wewe ndiye utakosa usingizi wao watakuwa wanakoroma😅😅😅
Ukiambiwa ya watu changanya na yako ila lililo la THAMANI sikiliza MOYO UNATAKA NINI na hapo utachagua njia ikupelekayo kwenye AMANI yako😎
Mama wa yote Haya MSIMAMO💪
#Elista_Kasema_ila_Sio_Sheria 🔨


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/02/yajue-mambo-yanayoua-mahusiano-na-ndoa.html

No comments:

Post a Comment