Tuesday, February 25, 2020

ZIJUE AINA NNE ZA KILIO CHA MTU KWENYE MAPENZI;



Image result for JINSI YA KUMNYONYA MATI-TI MWANAMKE
1. Mtu kulia ili kutafuta huruma kwa mwenza wake.
2. Mtu kulia kwa sababu anahisi anaonewa na mwenza wake.
3. Mtu kulia kwa hasira kwani anajutia kwa alichofanya.
4. Mtu kulia kwa woga wa kumkosa mwenza wake.
Vyote hivyo ni vilio ambavyo mtu hulia mbele ya Mtu, vilio hivyo vyote ni vya mtu KUJIHAMI... Mtu anapokuwa anajihami anakuwa na mambo makuu mawili kichwani mwake;
1. HAPENDI KUACHWA.
2. ANAPUNGUZA NGUVU YA
UGOMVI.
Kuna wakati mtu huyo unaweza kumtaja ni mwingi wa upendo ila kuna wakati unaweza kumtaja ni mtu asiye na upendo ila ni mwenye mazoea, Kwanini nasema hivyo? Mwenye UPENDO ni mwoga wa ugomvi pamoja kelele ambazo zitaharibu furaha yake japo MWENYE HUPENDO HASUBIRI MPAKA AKOSOLEWE bali hujitenga na makwazo kwa mwenza wake, Mwenye MAZOEA huishi kwa kuitegemea Faraja aipatayo kwa mwenza wake hivyo hapendi kuikosa japo ujinga wa hili ni pale mtu anapokuwa mzembe kiasi kwamba anaishi kwa kuona mwenza wake ni mdhaifu na asiye na ujanja wa kujitenga nae, Nini maana ya KULIA? Kulia ni kuondoa fundo moyoni, Mwache akulilie ili aondoe fundo moyoni lakini usikubari kilio hicho kikakuondoa kwenye MSINGI uliomtoa machozi, Nguvu ya MACHOZI imewaangamiza wengi, Ndo maana wahenga wakasema "UKITAKA KUMUUA NYANI USIMTAZAME USONI" Huruma kiasi huiachia uhuru akili ili kupambanua mambo, Lakini unapokuwa na Huruma kupita uwezo wako wa kukabiliana na tatizo UNAJIWEKA KWENYE MATESO YA KUDUMU... Sio kila chozi lina maanisha HUZUNI wengine kulia kwao ni jadi.


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/02/zijue-aina-nne-za-kilio-cha-mtu-kwenye.html

No comments:

Post a Comment