Thursday, February 27, 2020

πŸŒ·πŸ’•*DONDOO 20 ZA KUJENGA NA KUDUMISHA NDOA YENU*πŸ’•πŸŒ· 🌹

πŸ‘‰πŸ» *1. Kuaminiana, kuungana mkono, kusaidiana na kuwa na mtazamo chanya juu ya mwenzako* .
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *2. daima mridhie mwenza wako na umfanye ahisi kuwa ni mtu maalum.*
πŸŒ·πŸ‘‰πŸ» *3. Kuwa mcheshi, mburudishaji, kuwa wa maana na mwenye heshima kwa mwenzako* .
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *4. Kamwe usifukue makaburi ya makosa yenu ya zamani. Fikiria kuhusu leo, usiendelee kulilia yaliyopita.*
πŸ₯€πŸ‘‰πŸ» *5. Mhamasishe na umpe matumaini mwenza wako.*
πŸ₯€πŸ‘‰πŸ» *6. Usimlinganishe mwenzako na watu wengine hata kwa vitu vidogo.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *7. Mshangaze mwenza wako kwa mambo mapya.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *8. Pendeleeni kukaa pamoja kadiri inavyowezekana.*
πŸ₯€πŸ‘‰πŸ» *9. Daima jiandae kwa ajili ya mwenza wako na uwe na muonekano maridadi kwa ajili yake.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *10. Msikilize mwenzako, usimkatishe anapoongea. Heshima bora kabisa kwa mwenzako ni kumsikiliza anapoongea, hata kama jambo analoongea hukubaliani nalo, MSIKILIZE.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *11. Epukeni kupigana, kupuuzana, kuongopeana na kukasirikiana.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *12. Kuwa muwazi na umweleze mwenza wako wasiwasi na hofu yako kwa njia nzuri. Kumbuka: UKWELI HAUSEMWI VYOVYOTE WALA HAUSEMWI POPOTE.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *13. Kama mwenzako amekasirika, wewe kaa kimya angalau kwa sekunde 30.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *14. Epuka mabishano. Sema “kumradhi” hata kama kosa sio lako. Nusu shari ni bora kuliko shari kamili, na usalama wa ndoa yako ni bora kuliko ushindani unaoutaka.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *15. Daima iombee ndoa yako iwe imara na uhusiano wenu uwe madhubuti.*
πŸ₯€πŸ‘‰πŸ» *16. Daima uwe mwenye shukrani kwa mwenza wako.*
πŸ₯€πŸ‘‰πŸ» *17. Mwambie mwenzako “Nakupenda”. neno lisikosekane katika ndoa yenu.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *18. Kuwa muelewa kwa mwenza wako* .
πŸŒ·πŸ‘‰πŸ» *19. Hakikisheni macho yenu yanawasiliana mnapozungumza na kuongea.*
πŸŒΉπŸ‘‰πŸ» *20. Tengenezeni mazoea ya kula pamoja, kukaa pamoja na kusali pamoja.*

Image may contain: one or more people, people on stage and text


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/02/dondoo-20-za-kujenga-ndoa-yenu.html

No comments:

Post a Comment