Wednesday, February 26, 2020

Mwanaume Chunga Sana Hili ELIMU na UTAJIRI wako haivikufanyi wewe kuishi maisha mazuri


Image may contain: 4 people, people standing
📂Maisha yako yanaweza kupoteza muelekeo ghafla pindi utakapoanzisha mahusiano au kuoa.

📂Maisha yako yanaweza kuyumba kiuchumi pindi utakapoanzisha mahusiano au kuoa.

📂Haijalishi una nguvu kiasi gani kwenye uchumi na elimu, lakin nguvu hizo zitaathiriwa ghafla na aina ya mwanamke utakaye ishi nae.

📂Utasoma sana, Utakua na pesa nyingi, Elimu yako na Uchumi wako vitakufanya uonekana mpumbavu na mjinga kutokana na aina ya maisha utakayo yachagua.

📂Suala la kuoa ni suala la kutafakari kwa mapana sio kukurupuka, Unavyooa unaongeza mtu kwenye maisha yako hivyo hivyo mtu huyo anatakiwa aongeze kitu kwenye maisha yako.

📂Sio unaingia kwenye mahusiano unafilisika, au unaoa unaanguka kiuchumi elimu yako inakuwa haina msaada kwenye maisha yako.

📂Haijalishi mwanamke utakayemuoa atakuwa vipi labda hana elimu wala kipato lakini akiwa akili ya kufikiri kwa upana juu ya maisha yenu basi anaweza akaongeza utajiri wa mawazo kwako.

📂Usipende mwanamke wa kusema YES kwa kila utakachoamua, huyo mwanamke atakupotezea muelekeo, mpende mwanamke anaekupa challenge penda mwananke anayekukosoa.

J4REAL


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/02/mwanaume-chunga-sana-hili-elimu-na.html

No comments:

Post a Comment