π£ππππππππππππππ
_Inauma Sana Kuachana na Mtu ambae Unampenda Awe Mke/Mme au Mchumba, Maumivu yake hayaelezeki.ππ
_Chakula hakipiti, wala Usingizi haulaliki._
_Wakati mwingine kutokana na Maumivu makali ndani ya Moyo Kama hauna Khofu ya Mungu unaweza kujikuta unakufuru._ππ
_Unaweza kutamani uhame Dunia hii ukaishi ulimwengu mwingine._ππ
_Na hata kila ukijaribu kumsahau Unashindwa picha yake na Matukio mliofanya yanakuijia kichwani kila sekunde._ππ
_Moyo nao hautaki kumsahau._
_Nataka nikwambie Ndugu yangu wewe siyo kwanza kuumizwa Kihisia wala siyo wa kwanza kuachwa._ππ
_Ukikutana na Hali kama Hiyo Fanya yafuatayo._ππ
_KUBALI KUWA UMEPOTEZA NA CHUKULIA KAMA HUYO ALOKUACHA/MMEACHANA AMEKUFA NA MTU AKIFA HUWA HARUDI._ππ
_WEKA IMANI YAKO KWAMBA HUYO ALOKUACHA ALIKUWA HANA KHERI NA WEWE ANGEKUWA NA KHERI BASI ANGEBAKI._ππ
_KUWA NA SUBRA NA MUOMBE MOLA WAKO AKUPE MTU SAHIHI._ππ
_Kumbuka Unaweza Kuzani jambo lina kheri kwako na kumbe lina Shari kwako na Unaweza kuzani jambo lina Shari kwako na Kumbe lina kheri kwako._ππ
_Kila Unachohisi kizuri Ulichopoteza basi tambua kilikuwa haki kheri kwako.
ππππππππππππππ
source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/02/kama-umewahi-kupenda-utanielewa-na-kama.html
No comments:
Post a Comment