Wednesday, March 25, 2020

WANAWAKE LEO NGOJA NIWAAMBIE SIRI YA MWANAUME YEYOTE KUKUPENDA SANA.

Baadhi ya wanawake bado hawajajua kuwa usafi ni kivutio kikubwa kwa mwanaume, na kama tunavyojua kuwa usafi maana yake ni "kila kitu kuwa mahali pake”.
Si jambo jema kuweka mazingira ya nyumba yako rafu, vijiko vya chakula vipo kwenye kitanda eti kwa sababu tu una mtoto mdogo, au nguo za mikojo ya mtoto unaweka chini ya kitanda mpaka zinaanza kutoa harufu, hiyo haifai. We kama mke thihirisha ubora wako kwa kuhakikisha nyumba yako inakuwa kivutio cha mumeo kwa usafi wake.
Acha kujiachia eti kwa kuwa amekuweka ndani, endelea kupendeza kila siku kama alivyokukuta kipindi hajakuoa. Usiifanye ndoa yako ikazoeleka na kupoteza utamu wake kwa uchafu wa mwili na nyumba yako. Hakikisha unateka akili ya mumeo kwa kujiweka maridadi wakati wote.
Chris JR.


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/wanawake-leo-ngoja-niwaambie-siri-ya.html

No comments:

Post a Comment