Tuesday, March 31, 2020

NAOMBA NISEME TU KITU KIMOJA LEO. MNIVUMILIE LAKINI NAWASAIDIA. MAANA MMEZIDI.

Wanaume wengi huwatumia wanawake wazuri... - Dokta Joe Mapenzi ...
HII MSG SIJAANDIKA MIMI KUNA DADA KAANDIKA KASEMA NIMSADIE KUFIKISHA HUU UJUMBE
Kuna hii tabia mumeo mpenzi anakuambia mamii twende out for dinner.
Sasa shoga yangu sijui unakuwa na shida gani...
Ukiambiwa dinner maana yake ni utoke sexy.
Uvae nguo fulani hivi za kukufanya mwepesi. Uvutie.
Maana raha ya Dinner ukirudi home unaraha zoote mkifika tu home mnafanya finishing.
Sasa wewe sijui kungwi wako nani...
Unaambiwa dinner inaanza kuvaa mjitenge wako wenye stif kama tausi.
Lemba kubwaaaaaa....
Mara mikono mikubwa kama mwavuli...
Limkono la kitenge linaingia kwenye sahani ya chakula.
Weweeee.... Umeambiwa unaenda kwenyw mkutano wa Wabunge wa East Africa ama ?
UNAINGIA HOTELINI WATU WOTE WANAKUSHANGAA NA MTENGE WAKO KAMA MOVIE YA COMING TO AMERICA.....
Mume akinogewa akikugusa mahali anakutana na mstifu mkubwa tena wenye waya... jamaniii.. kheeee...
Akikugusa mgongo anakutana na mjistifu na sponji kubwaaaaa...
Una shida wewe.
Wakipita wake wa wengine unaanza kuoata hasira mumeo akigeuka.. inahusu.
Mtoto mdogo wa miaka 27 umevaa mjitenge utafikiri unawakilisha Mashindano ya vitenge Brazil... aaa bwana msinichoshe mimi.
Sasa bora basi mtenge tu. Kheeee. Na mjipochi mkubwaaaa.. utafikiri unaenda kuhesabu kura kama Mitimingi... (penzi kitovu cha uzembe)
Hivi hujui dinner ukialikwa ni jambo ambalo liko sexy???
Hahahahahahahahahaha.
Sasa umealikwa dinner unaanza... oooo naomba tuongeeeee...
Hahahahahaha.
Kabla hujaruhusiwa unaanza kama kweli unanipenda fungua simu yako. Nipe password..
Niambia Zulfa ni nani...
Nataka gari....
Na wewe si umtoe dinner yako ya hizo needs zako.. woiiiiii.
Akiputa dada na gauni lake na marashi yake unanuna.... unamnunia nani?uliombwa uvae miwaksi yako na mistifu pyeeeee.
Hahahahaha.
Umealikwa dinner.... hahahahaha... unaanza oo nataka safari lager... pyeeee...
Mnaniaibishaga jamani. Woiiiiii.
MUME ANATAKA KUKUSHIKA KICHWA ETI OO UTAVURUGA GERE LANGU...
Yale malemba ya kinaijeria.. hahahahaha. Shogaaa una shida. Dinner na lemba?
Hhahahahahahahaha.
Khaaaaa.
Yale malemba kabae harusini. Tena harusi ambayo unahusika na utaitwa mbele kulishwa keki. Hahahhaahahaha. Shangazi mtu... mama mdogo mtu ... hahahaha.
Sio keki hulishwi mume kapiga kitu cha uhakika unakazana na mjitemge wako wa stifu ..... Big noooo.
Saa ya kucheza mziki ukiambiwa ukacheze na hubby unaona hata aibu kusimama na kitenge chako. (Shona basi hata cha kijanja)
Maana saa ya mziki akishika kiuno akifikie.. akishika bega aliikie.. hahahahaha. NAWAZA MISTIFU YA VITENGE KIUNO ANAKIFIKIA SAA NGAPO.
MSHONO WAKO WA YAKE MABEGA FULANI YA VITENGE NAWAZA ANAFIKIA SAA NGAPI BEGA.
Hahahahahhahahaha.
MUME ANAKUAMBIA NINAKUTOA DINNER MAMII... Sasa sijui ni kutoelewa ama nini....
UNAANDAA WATOTO NA MASWETA. Hahahahahaha. ETI UPENDO. SIENDI MAHALI BILA WATOTO WANGU.
Hahahahahahahaha.
Khaaaaaa.Shikamooni.
Yani kusema a ukweli mnaniangushaga.
Nafanyaga ziara zangu nikiwa na mr...
Nakuta mtu kagharamiwa dinner hotel nzuri kanuna kama sijui nini.
Hahahahahahaha.
ANALIPA UNAANZA...
"yani ona unavyochezea pesa.. hunaplan kabisa. Pale Grocery ya Joseph bia si elfu 2500/=
Hapa unalipa bia 6000/=
Yani chakula hapa elfu 35000 sahani kwa kipi?
Pale twiga so tungekula mchemsho elfu 12 wote na tungeshiba...
Ulivyo lishamba unasindikiza hiyo sentensi na msonyooo....
Hahahahahahahaha.
NAWAZA...
UMEVAA MJITENGE WAKO WA STIFU ZA WAYA.
UMEKUNYWA SAFARI 4+MAANA UNAKOMOA.
ALAFU UNA HASIRA.
Hiyo sura siipatii picha.
Kama mgombea wa kiti fulani aliyeshindwa uchaguzi...
Hahahahahahaha.
Ukifika nyumbani sasaa...
Hugusiki wewe..
Misonyo wewe...
Mibeuo ya bia wewe...
Hahahahahaha.
Hasira wewe....
ACHENI KUFANYA MAISHA MAGUMU.
Na kina yakhe walivyo wachokozi sasa...Wakikuona na mjitenge wako wa stifu za waya na umekasirika maana mnanunaga...
Basi anapita pembeni yenu anasalimia..
Hi Mr Joseph alafu wewe anakuambia shikamooo...
Hahahahaha. Unasikiaje kupasuka moyo.
Ile nasemaga moyo unahama.
Unahamia Kwenye pua.
Hahahaha. Pumzi zinaziba. Hahahaahahahaha.
UKIONA WENZAKO WAMETUPIA TUVAZI TWAO TUNANOGA... MIMACHO KODI..
Unaanza Baba Ndetaulwa yule ni mke wake kweli?
Baba Bushiri mbona yule hajakusalimia?
Kheeeee..
ALAFU MUWAGE NA KAULI ZA MITOKO NA MAJINA YA WAPENZI WENU.
Mimi wangu namuitaga "Meli" Mambo ya honey.. bebi kila mtu woiiii.
Naitaga MELI full stop. Hahahahahahaha.
WATOTO WA SEKONDARI NA WANACHUO NDO WANAITAGA HONEY BEBI SWTY...WAKITAKA KUPEWA KITU.
Mimi sio mwanachuo. Hahahahahahaha.
MELI. Full stop.
KUNA WANAWAKE HUMU YANI MKITOLEWA DINNER AMA MKITOKA HARUSINI NYUMBANI HAMFIKI SALAMA. LAZIMA ZIPIGWE.
Hahahahahahahaha.
Acha kuvaa mavitenge yako ya stifu na waya uone dinner ilivyo sexy.
ETI KAMA UNANIPENDA NIAMBIE ZULFA NI NANI.Hahahahahahahahaha.
Dinner na Zulfa wapi na wapi.
Sasa ndo bahati mbaya apite hata jirani na kina zulfa.Mama yangu. Ngumi zinaweza kuanza ghafla. Malaya umekuja kunisanifisha.. washenzi wako... hao... umewaita waje kuniona...hahahahha. machozi debe. Moyo umehamia machoni. Hahahahahahahahaha.
WENGINE MOYO UNAHAMIAGA MIGUUNI NGUVU ZINAISHA MARA CHINI. UKIZINDUKA IPO HOSPITAL.
Dinner inageuka Pressure kisa mavitenge yako ya Stifu. Woiiiii.
KAMA UNANIPENDA NIFUNGULIE BOTIQUE.
Kama mimi mumeo nakujibu nakupa mtaji wa kwenda congo kununua vitenge.Maana ndo unavyopenda.
NAWAOMBA JAMANI NIPANIKISHIENI HAO MAKAHABA PLEASE.
Akija kusalimia akikuambia shikamoo ukiitikia marahaba mkono uwe kifuani mwa mumeo.
Yeye ndo moyo ukamhame huko.
Hahahahaha. Aanze UMENIFANYIA NINI?umekuja kunionyeshea na mkeo...
Hapo katuma msg... Na ndo kwanzaaa kamguu kwa chini inamkuna mr. Huku umemkumbatia.
Mr mwenyewe anamjibu...
NIHESHIMU NIKO NA WIFE.
ANAZIMA NA SIMU.
Ataisomaje namba???
Hhahahahahahahahaha.
Sasa nawaza mikono ya mwamvuli ukimkumbatia mume si kama amejifunika kitenge..
Mguu unanyanyaaje maana chini ni karibu kitenge kizima huo mshono.
Woiiiiiiii.
MNAFANYAG MAISHA YA NDOA KUWA MAGUMU. PYEEEE.
NDOA SI UTUMWA. NI KUJITUMA.
USIPOJITUMA INAKUWA NDOANO.
KWELI UNAALIKWA DINNER UNAPASI KITENGE CHA MSHONO WA TAUSI???serious???
Mnajua mnanitani?
Nikikukuta na mtenge wako dinani nakusalimia.
Nakuambia shikamoo. Uqche kuitika uone. (Ama mimi unanijua unaweza kuhisi natania.Nitatuma mtu akusalimie. Wacha nihamishe huo moyo.)


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/naomba-niseme-tu-kitu-kimoja-leo.html

No comments:

Post a Comment