Saturday, March 28, 2020

KWANINI MAHUSIANO NA NDOA NYINGI HUVUNJIKA BAADA YA SIRI ILIYOTUNZWA KUFICHUKA?


Kwanza ifahamike wazi MAPENZI IMANI kwa namna yoyote ile ni wajibu wa kila mmoja kujua IMANI ya mwenza wake kwake๐Ÿ’ฏ
Hatuwezi kuwa timamu kwa kila kitu lakini lipo kosa huhalibu IMANI katika mahusiano na ndoa zetu nalo ni;
• KUTOITUNZA AHADI ILIYOJENGA IMANI KWA MWENZA WAKO.
Ule mwanzo wa makutano huo ndo hubeba maana ya UHUSIANO WENU ila kama ulidanganya jambo ili kupata DHAMANA MOYONI MWA MWENZA WAKO niamini siku siri yako ikibaibika automatically MAPENZI YATAKUFA kwani ili Mtu ahisi UPENDO kwa mwingine ni pamoja na ANACHOKIAMINI KUISHI NAE.
Umemuaminisha MWENZA wako kwamba wewe UNAJIHESHIMU halafu anakuja kukubamba na NA MWINGINE hivi unataka ile IMANI YAKE KWAKO IENDELEE KUISHI?
Haitawezekana hata kama ANAKUPENDA VIPI maana DHAMANA YA UPENDO NI PAMOJA KUUISHI UHALISIA ULIOMVUTIA MWENZA WAKO ๐Ÿ’ฏ
Madhara makubwa katika mahusiano na ndoa ni pamoja na haya;
• UONGO.
• SIRI.
• UBINAFSI.
• KUJIHESABIA HAKI.
• UCHOYO.
Na mengineyo yanayofanana na hayo hayataweza kukomboa penzi lako
Maana halisi ya UPENDO ni kuwa MSAFI WA NAFSI kwamba usiwe na viashiria vya uchafu hapo utaweza kuutaja UPENDO.
Ni rahisi sana kuficha jambo ili umpate MWENZA wako japo gharama halisi ya hilo haitakuacha salama, Mahusiano na hata ndoa njia PEKEE ya kuyalinda haya ni pamoja na UWAZI kwamba kusiwe na aina yeyote ya kutokuwa mkweli, Japo wengi huamini ni udhaifu ila NAFASI YAKO ITABAKIA PALE PALE kuliko kama ungeficha halafu ukagundulika UTAPATA TAABU SANAAA๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
#Elista_kasema_ila_sio_sheria ๐Ÿ”จ


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/kwanini-mahusiano-na-ndoa-nyingi.html

No comments:

Post a Comment