Thursday, March 26, 2020

HUYAPONYI MAHUSIANO AMA NDOA YAKO KWA KUONYESHA KUNA MWINGINE ANAKUPENDA AU ANAFAA KULIKO UNAEDHANIA ANAKUUMIZA⛔


Matumizi mabaya ya WATSAAP pindi MAHUSIANO AMA NDOA inapoingiwa migogoro;
• KAMA UNAMPENDA KWELI EPUKA KUJIFANYA UNA FURAHA NA AMANI NJE YAKE KWANI HILO LITAGHARIMU DHAMANA YA UPENDO WAKE KWAKO ๐Ÿ’ฏ
Kumezuka tabia ya wana mahusiano pamoja na wana ndoa pindi wanapokuwa hawako kwenye maelewano kuanza kutunishiana kwa kutafuta namna ya kumfanya mwenza kushituka ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Mtu hata kama anaumia kwa DISTANCE iliyopo baina yao anatafuta ka picha kazuri akiwa anailazimisha FURAHA huku moyoni anayo MAJONZI ili tu mwenza wake aone eti bila yeye anayo AMANI๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Huko ni kulichawia penzi lako mwenyewe, Huwezi kujua ATHALI YA HIYO PICHA ITALETA GHARAMA GANI MOYONI MWA MWENZA WAKO๐Ÿ’ฏ
Kama kuna tatizo na kila mmoja anajaribu kujionyesha ana nguvu "KUTUNISHIANA MISURI" fahamu jambo moja;
• PENZI HUFA KWA VIKWAZO VIDOGO VIDOGO WALA SIO VIKUBWA.
Hakuna VITA YA MAPENZI ilidumu ikiwa wawili walopendana kuamua kuimaliza, Sio baba wala mama anaweza kuwa suruhu ya TESO LA MOYO ila mhusika wa PENZI HUSIKA.
Ukiona kuna tatizo hamjamaliza kwenye PENZI lenu basi asitafute makuu kwa kujifanya una FURAHA NA AMANI NJE YA MWENZA WAKO maana ni rahisi mno kulibomoa penzi kwa kujifanya hujali kilichotokea, Ni uongo kujifanya una FURAHA NA AMANI wakati mna tatizo kwenye uhusiano ama ndoa yenu, Tafuta AMANI KWENYE PENZI LA MOYO WAKO kuliko kutaka kujua Mwenza wako anumia kiasi gani baada ya kutofautiana nae ๐Ÿ’ฏ
USIYAJARIBU MAPENZI YAKO MWENYEWE kwa sababu kuna wakati yatageuka kuwa MWIBA MAISHANI MWAKO.
#Elista_kasema_ila_Sio_sheria ๐Ÿ”จ


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/huyaponyi-mahusiano-ama-ndoa-yako-kwa.html

No comments:

Post a Comment