Saturday, March 28, 2020

MUME WANGU BADO ANAWASILIANA NA MWANAMKE WAKE WA ZAMANI๐Ÿค”


Yalikuwa maneno mazito ya Msichana aliyejeruhika na NDOA yake baada ya kubaini Mumewe pamoja na kumuoa na kumhudumia kwa kila kitu lakini bado alikuwa anampenda Mwanamke mwingine ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ
Niliingia uhusiano na Mume wangu kwa muda wa mwezi mmoja na akaomba ridhaa yangu niwe mkewe, Ukweli ni kwamba sikuwa na sababu ya kukataa maana hata kwa kipofu kama angempapasa angebaini ni MWANAUME SAHIHI๐Ÿ’ฏ
Niliolewa kwa harusi nzuri tu, Mume wangu kwa matendo ni MWAMINIFU MNOOO lakini pia alinipa MUDA wake wote pamoja na kunihudumia kwa kila kitu, Kama Mwanamke sikuwa napungukiwa mahitaji yoyote, Maisha ya NDOA yangu yaliwavutia wengi hata wanawake wenzangu kusema;
" NIMEPATA FUTURE HUSBAND"
Ndoa yetu ilikuwa na FURAHA NA AMANI kwakweli sikujutia kuolewa wala Mume wangu sikutaka ajutie uwepo wangu, Maisha yetu kwenye NDOA yalitawaliwa na UAMINIFU kiasi kwamba hakuna alikuwa na mashaka na mwenzie, Hata hivyo nilijisahihisha kwa madhaifu yangu kabla Mume wangu hajajua kosa langu, Siku ya kufa nyani ikawadia kwa hakika nilitamani aridhi ipasuke nidumbukie humo๐Ÿ˜ญ
Tulikuwa sebuleni tumekaa tukitazama SULTANI ๐Ÿ‘‘ Kama kawaida tumekumbatiana ghafla simu yangu ikaita MSG mara Mume wangu akaidaka na kufungua msg ile kumbe ilikuwa ya SONGESHA.
Sikuwa na mashaka akanipa simu akasema ni SONGESHA wanataka usongeshe nikacheka nikamuuliza;
• MUME WANGU VIPI INGEKUWA YA MCHEPUKO?
Alijibu serious kwamba ANGENIKATA SHINGO nikabaki namcheka tu kwani tangu nimjue Mume wangu NILIFUNGA MUINGILIANO WA MAWASILIANO YA SIMU YA MWANAUME NJE YA NDUGU ZANGU tena anaowafahamu, Ghafla msg ikaingia kwenye simu yake, Mimi nikawa busy na SUMBURA ghafla nikaingiwa mashaka vile Mume anaandika msg nikampokonya simu, Nilichokiona kwenye simu ya Mume wangu kama ungekiona wewe UNGENIFIA KWA HOFU ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ
Ujumbe aloandika Mume wangu ulisomeka hivi;
• I LOVE YOU MUCH
Neno I love you halikunishitua sana Jamani ila emoj ya  hii ndo ilikuwa israel mtoa roho ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ
Elista relief of Heart naomba ushauri wako nifanye nini?
Majibu yangu kwa Mrembo huyu yalikuwa mafupi sana;
• UPENDO HUWA HAUGAWANYIKI MAANA YAKE MUMEO PAMOJA NA KUKUOA AMESHINDWA KUMUACHA EX NA BADALA YAKE AMEKUWA NA SABABU YA KUKUOA WEWE ILA UPENDO HALISI WAKE UPO NJE YAKO ๐Ÿ’ฏ
Kwenu wasomaji tumsaidie ndugu yetu kama wewe ungefanyaje?
#Elista_kasema_ila_Sio_sheria ๐Ÿ”จ


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/mume-wangu-bado-anawasiliana-na.html

No comments:

Post a Comment