Saturday, March 28, 2020

UNAPOTAKA KUCHAGUA MWENZA WA MAISHA FUATA HATUA HIZI UTAPATA MTU SAHIHI

Unapotokea kumchagua mtu wa maisha yako changua akili ...then muonekano ufuate ...
Chagua bidii ya upendo anaojaribu kukuonyesha .. Chagua bidii ya maisha anayojaribu kupambana nayo kila siku... Mtu mvivu atakuwa mzigo kwako.
Chagua utu uliomo ndani yake ..maana utu ukikosekana hatakuwa na huruma na wewe.
Chagua heshima anayokupa ..maana utajivunia kuwa nae.
Chagua uvumilivu atakao kuvumilia wakati ambao utakuwa na wakati mgumu.
Chagua hofu ya Mungu iliyojengeka ndani yake ...anaweza kuwa hauzurii nyumba za ibada lakini ipo hofu ya Mungu ndani yake ...wapo watu wa namna hiyo.. Atakuhurumia, atakupenda, atafurahi anapokuona umeweka bidii katika kumtafuta Mungu.
Chagua ulinzi wa kihisia atakao kuwekea ..mtu ambae atajaribu kulinda hisia zako....ikitokea amefanya kosa atafanya bidii ya kukuonyesha yale yalikuwa ni makosa but mimi bado ni mtu mwema na bora kwako.


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/unapotaka-kuchagua-mwenza-wa-maisha.html

No comments:

Post a Comment