Tuesday, March 31, 2020

KATIKA HILI POLENI SANA WANAWAKE HAKIKA MNAPITIA MTIHANI MGUMU SANA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAZURI ZAIDI TANZANIA - Invidious
Kati ya mitihani migumu zaidi wapitiayo wanawake katika ndoa ni KUCHOKWA. Unakuta mwanzo mme alikua akija kutoka kazini mbwembwe kibao mara mabusu na sifa kibao mara hongera umependeza sana wife n. k ila baada ya mda hususani mwanamke akianza mambo ya UZAZI ambapo wengi hubadilika shepu na mvuto wao wa awali ndipo kizaa zaa na timbwili la asha ngedere linapoanza utasikia we mwanamke mbona wanuka mijasho ivo leo umeoga kweli?
Unakuta mwanaume anamkejeli mkewe eti hicho kitambi unamfugia nani? Amesahau kitendo cha mke kumzalia watoto ndio chanzo cha tumbo kutorejea katika hali yake na kuonekana kama kitambi.
Natamani kila mwanaume leo hii angefikiwa na ujumbe huu ausome ajifunze atambue JINSI MKEWE ALIVYO CHANZO NI YEYE abadilike amuheshimu mkewe na kumjali asimdharau kwa mabadiliko ya muda ya kimwili yatokanayo na uzazi, ndugu msomaji kama unaguswa kwa namna moja au nyingine na ujumbe huu andika IMEPENYA HIYO kisha SHARE ujumbe huu uwafikie wanaume wote nchini.
Nakutakia siku Njema, Mungu Akubariki na kukulinda


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/katika-hili-poleni-sana-wanawake-hakika_31.html

No comments:

Post a Comment