Tuesday, June 16, 2020

USIUDANGANYE MOYO WAKO KWAMBA ULIYE NAE MNAENDANA KISA ULIPENDA UWE NA MWENZA ALIYE SMART KESHO NI FUMBO πŸ€”


Muonekano unaweza kupotea kwa hali ya maisha kubadilika ama ugonjwa na wakati mwingine umri nao ni sehemu ya badiliko la MUONEKANO.
Unaweza kuamini kwa macho lakini ikawa sio vile NAFSI YAKO INAHITAJI na tatizo limewapata wengi, Unamtazama Mtu na kuamini kuwa ni yeye pengine ni kwa sababu tu ana sifa mbili kati ya zile ulipenda awe nazo MWENZA WA MAISHA YAKOπŸ’‘
Haja ya nafsi haitafutwi kwa majaribio, lakini pia kumbuka wazi ULIVYO LEO UNAWEZA KUWA BORA ZAIDI BAADAYE ukajikuta unamuona mwenza wako haendani nawe tena na hapo utanielewa nikisema MUONEKANO WA MTU SIO HITAJI LA NAFSI ila ni ukosefu wa utulivu wa HISIA ZAKO.
Mchukuwe Mtu aliye chaguliwa na NAFSI YAKO halafu mjazie mapungufu yake, Mfanye awe kamili kama ulivyohitaji Mwenza wako awe, Ndo maana ni rahisi kwa Mwanaume kuwa na MWANAMKE WA NAFSI YAKE kuliko Mwanamke kuwa na Mwanaume wa NAFSI YAKE sababu ni ndogo sana:-
 Mwanaume kumuoa Mwanamke na kwenda kumtengeneza ni rahisi, kuliko Mwanamke kuchukuwa Mwanaume wa HISIA zake na kwenda kumtengeneza, Kwani tamaduni zetu zitamfanya Mwanamke huyo kuonekana ANAMHONGA MWANAUME wakati huo Mwanaume kumhudumia Mwanamke ni wajibu hata vitabu vya dini vimeagiza hilo.
Kwa sababu hiyo WANAWAKE wengi wanaolewa na wanaume wasokuwa wa NAFSI ZAO kwa sababu pamoja na Mwanamke kupenda Mwanaume SMART lakini pia kumkuta Mwanaume ameji-bland mwenyewe ni USHINDI Kwani Hawa viumbe nao UNAWEZA KUMTENGENEZA ukanyanganywa na SHOST πŸ˜‚πŸ˜‚
Halafu Mwanaume HAFUGIKI kama hujui Jaribu KUMFUGA UJE KULIA🀸‍♂️🀸
utamuzaidiapp


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/06/usiudanganye-moyo-wako-kwamba-uliye-nae.html

No comments:

Post a Comment