Monday, June 15, 2020

TATIZO KWETU ANAJULIKANA Je na wewe ni miongon mwa WASICHANA ambao wanalilia penz lililo kwisha yumba kisa tu wazaz au ndugu?

TATIZO KWETU ANAJULIKANA
Je na wewe ni miongon mwa WASICHANA ambao wanalilia penz lililo kwisha yumba kisa tu wazaz au ndugu?
" Nashindwa kumuacha maana alikuja kwetu hivyo wazaz wangu wanamfahamu
Naogopa nikimuacha nitaitia aibu familia yangu hata mimi pia"
NIKUULIZE SWALI
Kwa nin uogope kumuacha mwanamke au mwanaume kwa tabia zake chafu kisa ndugu wanajua mahusiano yenu?
Kipi bora umuache saizi au usubir kuhangaika kuivunja ndoa?
Dada acha kujiendekeza,kama yeye alikutambulisha lakin yupo ktk hatua za kuoa mwanamke mwingine kwa nini we ushindwe kuendelea na maisha yako?..
Aliye kuambia kuwa mtu akijulikana na wazaz hawez achika nan?
Zinavunjwa ndoa za kanisan na misikitin ndo iwe wewe uogope kumuacha wakat hata hujaanza kuishi nae,unaogopa nini?
ZINDUKA
Kama ulivyo mtambulisha mwanzo kwa ndugu au wazaz pia unaweza wambia kuwa huwez endelea na huyo mtu sababu kuna mambo hujaridhika nayo na yataifanya ndoa yako iwe chungu ukilazimisha kuishi nae
Wanawake wengi wanateseka ktk mahusiano kuwalilia wanaume wasio wataka kwa sababu ya kutoamin kuwa penz limekufa
Yaan mdada anajua fika kuwa kwa sasa hapendwi na mwanaume wake ana mwanamke mwingine,lakin mdada hujikuta akiendelea kusubir muujiza wa penz kurudi kama mwanzo.
Sikiliza
Ukiachwa achika
Usiogope maumivu ya mda mfupi
Usiishi ktk ndoto isiyo weza timiam kubali kuwa ametoweka ktk maisha yako,jipange upya kwa yajayo.
Hakuna aibu wala majuto kuachana na penz ambalo unajua kuwa linakuumiza na halina malengo mazur kwako.
Muache aende
We sio wa 1 kuvunja mahusiano
ACHA KABLA KUACHWA


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/06/tatizo-kwetu-anajulikana-je-na-wewe-ni.html

No comments:

Post a Comment