Monday, June 15, 2020

MAGUMU UNAYOPITIA SASA YANAKUANDAA.


Watu wengi hujinamia na kukaa wakilalamika ju ya mambo magumu wanayopitia ama kukumbana nayo ila Ukweli ni kwamba kila changamoto katika maisha Huwa na sababu yake.
Zingine Huja kwa uzembe wetu, zingine Huja kwa Juhudi za maadui zetu , Na zingine Huja kwa Mkono wa Mungu ili akupike vizuri, akuandae kuwa Mtu Fulani hapo baadae .
Usiumie Unapopitia changamoto, Jaribu kutabasamu na Kuzikabili ili ufikie Hatima ya mambo ulioyakusudia
Hata barabarani ukisema matuta na makorongo uyatazame Sizani kama unaweza ukapita.
Ila ili ufike unakokwenda ni Lazima uyakanyage tu.
Sasa fanya changamoto zako kama matuta tu Barabarani, umia kichwa namna ya kuzitatua ila usiumize kichwa kwa Jinsi zilivo kuu.
Changomoto ni fursa Ya mafaniko kwani hukuonyesha wapi ulikwama na kuteleza na Ufanye nini ili Upate unachotaka.
Kifupi Changamoto ni Majibu Ya Mafanikio Yako ya kesho na kesho kutwa.
Chukua hatua sasa!!!
utamuzaidiapp


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/06/magumu-unayopitia-sasa-yanakuandaa.html

No comments:

Post a Comment