Saturday, June 13, 2020

KAMA UPO KWENYE MAHUSIANO TAMBUA HAYA.


.Sanchi World Biography - Age, Model » » tooxclusive
πŸ‘‰ Sio Kila Mahusiano Ya kimapenzi kati Ya mwanamke Na mwaume Lazima yafikie hatua ya kuoana na kuwa mume na mke.
Mahusiano mengine yalipaswa kuwa ya muda mfupi tu ili mtu ujifunze, maisha yaendelee. Ni mahusiano machache sana ambayo ukomo wake huwa ndoa.
Hivyo ukiona umeachika huna haja ya kujiua Jaribu kuelewa hali halisi maisha yaendelee.
.
πŸ‘‰ Usimpende mwanamke au mwanaume ukatumbukia moja kwa moja mpaka nywele na miguu, mpende kwa kiasi fulani kwanza. Ila mpende Mungu Kwanza na umpe yeye kipaumbele kuliko kile unachompa mpenzi wako ambae ni binadamu mwenye siri na moyo kichaka,anachokuwazia inabaki siri nzito.
.
πŸ‘‰ Usimpende Mtu kwa sababu ya Uzuri wake, utanashati wake Au pesa zake.
Je unaweza kumpenda mtu huyo huyo hata kama akiwa masikini?
Au uzuri wake utakapo potea utaendelea kumpenda na kumheshimu?
Je yatokayo moyoni mwake yanaweza kukuweka (uzuri wa ndani) kama huwezi kumpenda mtu huyo kama vitu vya nje vikipotea basi bora muachane ufanye ishu nyingine maana hapo mnapoteza muda.
Mapenzi bora na ya kweli hayajengwi juu ya vitu na uzuri wa nje maana hivyo vinachakaa na kutoweka lakini roho iliyopenda hubaki ikichanua daima.
πŸ‘‰ Elewa, Upendo Pekee hautoshi kuimarisha na kulinda penzi lenu. Kujitambua, kuwa na Hekima Na uvumilivu ni Nguzo kuu katika Mahusiano na kujenga ndoa imara inayoketa furaha na hatima bora.
.
Kavolume kametosha au niongeze kidogo??


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/06/kama-upo-kwenye-mahusiano-tambua-haya.html

No comments:

Post a Comment