Thursday, March 19, 2020

Unafikiri ni Kwanini baadhi ya Wanaume wameshindwa kutambuwa THAMANI YA MWANAMKE?

Image may contain: one or more people
Mtazamo wa kwanza wa Mwanaume kwa Mwanamke ni USAFIπŸ’ƒ
Ndo maana Mwanamke anapokuwa hajaoga, hajavaa nguo nzuri, hajapaka mafuta ya kunukia na kujipamba ANAKUWA SALAMA ZAIDI KULIKO AKIISHA JIWEKA NADHIFU🀦🏾‍♂
Mwanaume ambaye anamtazama Mwanamke kwa USAFI WAKE na usafi ule akaupeleka moyoni mwake niamini Mwanaume huyo atakuwa amempa FURAHA MWANAMKEπŸ˜‚
Lakini Mwanaume asipoupeleka usafi wa mwanamke MOYONI Yaani ukakomea kwa macho ujue MWANAUME HUYO ATAENDELEA KUWATAZAMA WANAWAKE WENGINE AMBAO NAO NI WASAFI😭
Kwanini nasema hivyo;
Wanaume walio wengi humchukuwa Mwanamke kwa usafi kuliko Uzuri wake na hapo ndipo utatofautisha kati ya UZURI NA USAFI... Mwanaume ni Mtu mwenye tamaa by nature lakini nikiri kabisa wapo wanaume ambao tamaa zao HUTAMANI ALIPOPENDA NA ASIENDE KWINGINEπŸ’ͺ🏽
Hapa ndipo unapata maana kubwa mbili;
Mwanamke asimamie kile ambacho kilimvutia Mwanaume wala asilewe na upendo anaopewa kwa sababu kila kukicha MATOLEO MAPYA YA WANAWAKE YANAFYATULIWA🀣
Mwanaume aijue thamani na UTU wa mwanamke wake ili kumfanya mwanamke asiishi kwa masononeko hata akajikuta anakuwa mpwekeπŸ™†πŸΏ‍♂
Kila mmoja aijue sababu ya yeye kumpenda mwenza wake, Mwanamke asijione Mzuri bali ajue kwamba SIO KILA MWANAUME HUMPENDA MWANAMKE KWA UZURI WAKEπŸ’ƒ
Mwanaume asijione yeye ni zaidi ya wanaume wenzie kwamba Mwanamke huyu hawezi kumpata mwingine ila yeyeπŸ•Ί
UPENDO sio kitu bali ni maana ya uhitaji wa NAFSI 
Unaweza kuwa Mwanamke mzuri na usijue FURAHA YA MAPENZI NI NINI Kwani Uzuri wako watu wanautazama kama MIONDOKO YA PUNDAMLIAπŸ¦“ wala hawana kinachoshinda tamaa juu yako, Unaweza kuwa Mwanaume rijali lakini ukakosa Mwanamke wa kukupenda kwa hakika kwa sababu HAKUNA MWANAMKE ANAPENDA KARAHA
Kwa hiyo UPENDO ni MOYO na kama ndivyo ilivyo maana yake KILA MTU ANAPOKUWA ANAMPENDA MWENZA WAKE AHAKIKISHE ANASIMAMIA MISINGI YA UPENDOπŸ™‹πŸ»‍♂
Huwezi kumpata mtu mtimilifu kwa asilimia 100 ila ukimpata mtu japo ni mkamilifu kwa asilimia 40 mfanye ajitambuwe japo afikie 60% ili avuke nusu ya utimilifuπŸ™
Ni rahisi kumfanya Mpenzi wako kuyaishi yale upendayo ikiwa nawe unakubaliana na yale ambayo anapenda uyaishiπŸ‘Œ
Na hapo ndipo unaipata maana ya
"WAWILI WAKINIA MAMOJA NI SABABU KUBWA YA WAO KUTIMIZA ADHIMA YA PENDO LAO"
Shirikianeni kukataa MAFARAKANO lakini pia muwe na SHAUKU YA KUISHI PAMOJAπŸ‘«
Niamini MAPENZI YENYE UTULIVU HUSAHAULISHA DHIKI NA UGUMU WA MAISHA na hapo utagunduwa kwamba BIN ADAM TUNAHITAJIANA SANA... Basi nikwambie UHITAJI WENYE TIJA ULIOJENGWA NA MAPENZI huo ndo hunenepesha MOYO na kumsababisha mtu kuwa na NURU pamoja na FURAHA ILIYO TAWALIWA NA AMANI✌🏼
Nayapenda MAPENZI kwa sababu ni suruhu ya STRESS ZOTE KWENYE MAISHA YA BIN ADAMπŸ˜‹
#Elista_kasema_ila_Sio_SheriaπŸ”₯


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/unafikiri-ni-kwanini-baadhi-ya-wanaume.html

No comments:

Post a Comment