Sunday, March 22, 2020

JE ULIWAHI KUISHI KWENYE MAHUSIANO/NDOA NA MTU AMBAYE AMEKUFANYA KAMA DARAJA LA MAFANIKIO YAKE๐Ÿคท๐Ÿฝ‍♂

Unhappy Young Woman Having Argument With Man At Home Stock Photo - 55432731
Bin adam tuna tabia tofauti iwe kwa maumbile ama hulka za ki malezi, Upendo mwingi hugeuka kuwa teso kwa yule anayejitoa MWILI, AKILI NA MOYO WAKE kwa ajili ya kumpenda mtu... Sisemi TUSIPENDANE laa hasha๐Ÿคฆ๐Ÿพ‍♂ ni tendo linaloashiria UBIN ADAM japo hata viumbe wengine wanapendana Kwani hujawahi kuwaona kumbikumbi๐Ÿฆ—? Wapo watu hutamka NAKUPENDA kama ishara ya pumbazo kwa mwenza wake, Mtu anaweza kulia ama kujiuguza ukadhani MPENZI SI HUYU SASA lakini ni mhunzi wa MAPENZI FAKE๐Ÿ™†๐Ÿฟ‍♂
Kikubwa alichonacho pengine aliishajua NYOTA YAKO inapandisha maisha yake, Wakati unakutana nae hata muonekano hakuwa nao ila leo kila mtu anapomtazama anam-admare ๐Ÿ‘Œ swali je anakumbuka alikotoka? Wengi wenye tabia hizo hujihesabia haki kwani wamejawa ubinafsi, Mtu anapokufanya DARAJA la mafanikio yake kamwe hatajwi kwa upendo bali ni kwa masrahi yake, Watu hao kila ukitaka kumuacha TARAJIA KUONA PIPA LA MACHOZI๐Ÿ˜ญ
Lakini ukimpa kisogo tu ANAKUNG'ONG'A๐Ÿคฃ mtu huyo ni hatari kwa maisha yako Kwani iko siku ambayo haina jina ATAKUMWAGA HUTAAMINI Kwani anaweza kukuvumilia kwa sababu malengo yake hayajatimia ngoja atimize malengo yake utaita Mama na alishatangulia mbele za haki๐Ÿ˜Ž
Machozi hayatoki moyoni, Kilio cha kwikwii na huzuni nyingi hazitoki moyoni, MOYO wa mtu ni ficho la kile anachokipanga sasa wewe endelea kumuonea huruma mwenzio kwa masrahi yake aje atusue akumwage๐Ÿป ujutie kumvumilia wakati huo mwenzio atakuwa ANAIPEPERUSHA BENDERA๐Ÿšฉ ya penzi jipya na mtu ambaye hata hakumuombea kwa MUNGU kwa mafanikio aliyopata huku wewe ukiachwa UNAPAUKA TU๐Ÿ˜ kataa kuwa DARAJA LA MAFANIKIO Ya Mtu laa kama unaamini safari yenu ni moja, Muda ni mali isiyooza ila inapitwa na wakati, Sasa wewe endelea kubembelezwa ukidhani unapendwa kumbe mwenzio anatembelea NYOTA YAKO ๐ŸŽ‡
#Elista_kasema_ila_Sio_sheria ๐Ÿ•บ


source https://utamuzaidiapp.blogspot.com/2020/03/je-uliwahi-kuishi-kwenye-mahusianondoa.html

No comments:

Post a Comment